Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w95 12/1 uku. 32
  • Usifungie Kinyongo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usifungie Kinyongo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
w95 12/1 uku. 32

Usifungie Kinyongo

KUEPUKA kuwa na hasira mtu fulani atuudhipo huenda likaonekana kuwa jambo gumu zaidi. Biblia ina shauri lenye kutumika kwa hali kama hizo. “Mwe na hasira,” mtume Paulo akaandika, “ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka.”—Waefeso 4:26.

Mtu fulani akitukosea, ni jambo la kawaida kuwa na kiasi fulani cha hasira. Jambo la kwamba Paulo asema “mwe na hasira” ladokeza kwamba nyakati nyingine huenda hasira ikastahili—labda likiwa tokeo la kutendewa isivyofaa au kutotendewa kwa haki. (Linganisha 2 Wakorintho 11:29.) Lakini ikiachwa bila kusuluhishwa, hata hasira inayostahili inaweza kuwa na matokeo mabaya, ikiongoza kwenye dhambi nzito. (Mwanzo 34:1-31; 49:5-7; Zaburi 106:32, 33) Hivyo, unaweza kufanya nini uhisipo kwamba umeudhiwa hata ukakasirika?

Katika visa vingi vinavyohusu makosa madogo-madogo, unaweza ama kusuluhisha hali hiyo moyoni mwako “na kutulia” au umwendee mwenye kukuudhi na kuzungumzia jambo hilo. (Zaburi 4:4; Mathayo 5:23, 24) Kwa vyovyote, ni afadhali kusuluhisha jambo hilo haraka ili kwamba hasira isiongezeke na kutokeza matokeo yenye msiba.—Waefeso 4:31.

Yehova husamehe makosa yetu kabisa, hata dhambi ambazo huenda tusijue tumetenda. Je, hatuwezi vilevile kusamehe makosa madogo ya binadamu mwenzetu?—Wakolosai 3:13; 1 Petro 4:8.

Kwa kupendeza, neno la Kigiriki la “samehe” kihalisi lamaanisha “kuachilia.” Msamaha haudai kwamba tupunguze au turuhusu kosa. Nyakati nyingine huenda tu ukamaanisha kuachilia hali fulani, ukitambua kwamba kufungia kinyongo kutakuongezea tu mzigo na kuharibu muungano wa kutaniko la Kikristo. Zaidi ya hayo, kufungia kinyongo kwaweza kuathiri afya yako!—Zaburi 103:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki