‘Je, Mungu Ananijali?’
“JE, YEYOTE Hunijali? Je, Mungu Hujali?” Ndivyo kilivyosema kichwa cha makala moja iliyotokea katika Christianity Today. “Sehemu kubwa ya kazi yangu nikiwa mwandikaji imehusu tatizo la uchungu,” asema Philip Yancey, mwandikaji wa hiyo makala. “Mimi hujiuliza tena na tena maswali ayo hayo, kana kwamba nagusa kidonda ambacho hakiponi kamwe. Mimi husikia kutoka kwa wasomaji wa vitabu vyangu, na masimulizi yao yenye uchungu mwingi huthibitisha shaka zangu.”
Labda wewe pia umejiuliza ikiwa Mungu anapendezwa na maisha yako. Aha, labda unafahamu Yohana 3:16, lisemalo kwamba “Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee.” Au huenda ukawa umesoma Mathayo 20:28 (New World Translation), lisemalo kwamba Yesu alikuja “kutoa nafsi yake kuwa fidia katika kubadilishana kwa ajili ya wengi.” Na bado waweza kuuliza, ‘Je, Mungu hutoa uangalifu kwangu mimi? Je, yeye hunijali mimi binafsi?’ Kuna sababu nzuri ya kuamini kwamba yeye hujali, kama tutakavyoona.