Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 8/15 kur. 2-3
  • Kuzuru Bara Lililoahidiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzuru Bara Lililoahidiwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Mtaigawa Nchi Iwe Urithi’
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Je, Una Sababu ya Kuamini Kwamba Kutakuwa na Paradiso?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Masomo Yenye Kutumika Kutokana na Bara Lililoahidiwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Funzo Namba 1—Ziara Kwenye Bara Lililoahidiwa
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 8/15 kur. 2-3

Kuzuru Bara Lililoahidiwa

TUSEME rafiki angekuambia kwamba alikuwa amekununulia—zawadi—nyumba mpya kabisa katikati ya mazingira mazuri na matulivu. ‘Yaonekanaje?’ ungejiuliza. Bila shaka ungekuwa na hamu ya kujionea nyumba hiyo, kutembea ndani yayo na kuchunguza kila chumba. Kwani, hayo ndiyo makao yako mapya!

Katika 1473 K.W.K., Yehova alilipatia taifa la Israeli la kale makao mapya—Bara Lililoahidiwa, ukanda wa eneo la karibu kilometa 500 kutoka kaskazini hadi kusini na upana wa kilometa 55, kwa wastani.a Likiwa katika mahali ambapo pameitwa Hilali (Eneo) Yenye Rutuba, lile Bara Lililoahidiwa lilikuwa mahali pa kuishi penye kupendeza, palipobarikiwa na hali zalo zenyewe za pekee.

Lakini kwa nini wapasa kupendezwa leo na “makao” aliyopewa mtu mwingine, hasa mtu aliyeishi muda mrefu uliopita? Kwa sababu ujuzi juu ya bara hilo la kihistoria waweza kuongeza uthamini wako wa masimulizi ya Biblia. “Katika bara la Biblia,” akaandika Profesa Yohanan Aharoni aliyekufa, “jiografia na historia zimechangamana sana hivi kwamba hakuna moja iwezayo kueleweka bila msaada wa ile nyingine.” Zaidi, katika upeo walo, Bara Lililoahidiwa liliandaa kielelezo kwa kadiri ndogo cha kile ambacho Paradiso chini ya Ufalme wa Mungu itamaanisha kwa wanadamu ulimwenguni pote!—Isaya 11:9.

Wakati wa huduma yake ya kidunia, Yesu Kristo alitumia mandhari za kawaida katika Bara Lililoahidiwa ili kufundisha masomo yenye kutumika. (Mathayo 13:24-32; 25:31-46; Luka 13:6-9) Sisi pia twaweza kujifunza mengi kwa njia yenye kutumika kwa kuchunguza mambo mbalimbali ya Palestina ya kale. Hivyo acheni tutembee kupitia baadhi ya vyumba vyayo, kwa kusema kitamathali, tukichunguza baadhi ya mambo yenye kutokeza ya bara hili lililokuwa makao ya watu wa Mungu kwa karne nyingi. Kama tutakavyoona, kuna mengi tuwezayo kujifunza kutokana na Bara Lililoahidiwa.

[Maelezo ya Chini]

a Utumizi wa maneno “Bara Lililoahidiwa” katika makala hizi waona mambo kulingana na nyakati za kale, jinsi yalivyo katika Biblia, na bila kuhusika katika madai ya kisiasa na ya kidini katika hilo eneo.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 2]

Cover: Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 3]

Garo Nalbandian

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki