Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 9/1 uku. 32
  • “Usiwafukuze!”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Usiwafukuze!”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 9/1 uku. 32

“Usiwafukuze!”

“IWAPO mmoja wa Mashahidi wa Yehova, au hata wawili, apiga kengele ya mlango wako, usiwafukuze!” lashauri gazeti la habari Corriere della Sera. Hilo gazeti la habari lilikuwa likirejezea jambo fulani lililotendeka katika Treviso, kaskazini mwa Italia, ambalo katika hilo mfanya biashara mmoja alikuwa karibu kupoteza zaidi ya lire milioni moja (zaidi ya dola 600 za Marekani) kwa sababu ya kuwafukuza Mashahidi wawili waliomtembelea.

Kulingana na gazeti hilo la habari, Mashahidi wawili walijitambulisha kwa mtu huyo kwa maneno: “Leo ni siku nzuri kwako. Sisi ni Mashahidi wa Yehova, na tuna kitu fulani chenye thamani cha kukupa.” Ndipo, huyo mfanyi biashara asiye mwenye urafiki akaufunga mlango, bila kuwaruhusu wamalize ujumbe wao.

Ikiwa huyo mtu angalisikiliza, angalipata kujua kwamba hao Mashahidi walikuwa wameenda nyumbani kwake ili kurudisha kibeti chake, walichokuwa wamekipata kwenye benchi la bustani. Kwa hiyo hao Mashahidi hawakuwa na la kufanya ila kupeleka hicho kibeti pamoja na yaliyomo kwenye kituo cha polisi cha karibu zaidi. Siku iliyofuata, polisi walikirudisha kwa mwenyewe.

“Ikiwa mtu mwingineye angalikuwa katika hali ya wale [Mashahidi] wawili wasiofanikiwa,” likasema gazeti la habari Il Gazzettino di Treviso, “labda . . . angaliweka kile kiasi kikubwa cha fedha kilichokuwa katika kibeti hicho. Lakini si Mashahidi wa Yehova, ambao wapaswa kuwa wenye kufuatia haki kikamili.”

Ni nini kinachowasukuma Mashahidi wa Yehova “kuwa wenye kufuatia haki kikamili”? Ni upendo wao kwa Mungu na kwa jirani, kwa kupatana na mafundisho ya Yesu Kristo. (Mathayo 22:37-39) Hiyo pia ndiyo sababu inayowafanya Mashahidi wa Yehova waende nyumba hadi nyumba ili kutangaza habari njema kuhusu ile “dunia mpya” nzuri ajabu iliyoahidiwa na Yehova Mungu. Ujumbe huo wenye tumaini ni wa thamani zaidi sana kuliko mali yoyote ya kimwili!—2 Petro 3:13, HNWW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki