Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w96 10/15 uku. 32
  • “Yehova Alijibu Sala Zangu!”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Yehova Alijibu Sala Zangu!”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
w96 10/15 uku. 32

“Yehova Alijibu Sala Zangu!”

ULIMWENGUNI pote, Mashahidi wa Yehova wanaongoza mafunzo ya Biblia nyumbani yapatayo milioni tano pamoja na watu wanaopendezwa kupata ujuzi sahihi juu ya Mungu na makusudi yake ya ajabu kwa ajili ya wanadamu. Hata watoto miongoni mwa Mashahidi wa Yehova wanashiriki katika kazi hiyo. Kwa kielelezo, fikiria mvulana aitwaye Joel. Yeye alibatizwa alipokuwa na umri wa miaka tisa kwa kufananisha wakfu wake kwa Yehova. Mwaka mmoja baadaye aliona jambo hili:

“Nilipokuwa katika huduma, nilimkuta mwanamke aitwaye Candy. Nilimtolea ile broshua ‘Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.’ Tayari alikuwa nayo, kwa hiyo nikamtolea kile kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Tayari alikuwa nacho pia. Kisha nikafikiri, ‘Nitamtolea mwanamke huyu funzo la Biblia.’ Akakubali!

“Dada ya Candy, aliyekuwa mahututi kwa sababu ya kansa, akaja kuishi naye. Kwa kuongezea, Candy alikuwa akisomea uuguzi. Kwa hiyo kwa kipindi fulani cha wakati, funzo la Biblia likaachishwa. Lakini wazazi wangu nami tuliendelea kuwasiliana naye kwa kumwachia yeye au mume wake, Dick, magazeti. Alituambia kwamba aliyaweka hayo magazeti kando ya kitanda chake na alikuwa akiyasoma usiku.

“Hatimaye, dada ya Candy akafa. Baba yangu na mama yangu nami tulizungumza na Candy juu ya hali ya wafu. Akaamua kuanza tena funzo lake la Biblia. Kwenye siku tofauti, tulimuuliza Dick ikiwa angependa kujifunza pamoja na Candy na kulifanya liwe funzo la familia. Akaliona kuwa wazo zuri. Kwa hiyo sasa, nikiwa na baba yangu, ninajifunza na Dick na pia Candy. Wanafanya maendeleo mazuri na wanaonyesha uthamini kwa ajili ya funzo la Biblia.

“Nilikuwa nikisali nipate funzo la Biblia, naye Yehova alijibu sala zangu!”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki