Je, Tutapata Wakati Wowote Kuondokewa na Mandhari Kama Hii?
POPOTE tugeukapo siku hizi, twaona udhihirisho wa uvutano, pambano, na vita. Kusudi la gazeti hili si kuongezea habari zote mbaya unazojua tayari. Badala ya hivyo, toleo hili la pekee litakujulisha angalau kweli mbili zenye kufariji. Kwanza, kwamba unabii mbalimbali wa kale katika Biblia ulitabiri sehemu kubwa ya habari mbaya zenye kushtua za enzi yetu; pili, kwamba kitabu hichohicho cha unabii hutabiri siku ambayo katika hiyo mandhari zinazofanana na hii ambayo imeonyeshwa hapa zitakuwa za wakati uliopita. Hakuna vita tena. Hakuna milipuko ya mabomu, wapiga-risasi stadi kutoka mafichoni, mabomu ya kutegwa chini ya ardhi, wala uharamia tena. Hakuna mayatima wenye maumivu makali au wakimbizi wasio na makao tena. Ulimwengu wenye amani ya kweli, yenye kuufariji moyo. Je, ungependa kuona wakati kama huo? Twakusihi sana uchunguze yale ambayo Biblia husema. Waweza kupata faraja zaidi katika Biblia kuliko vile ulivyopata kufikiri yawezekana wakati wowote.