Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 7/1 uku. 32
  • Mashahidi wa Yehova Wanapozuru

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Wanapozuru
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 7/1 uku. 32

Mashahidi wa Yehova Wanapozuru

Wakatoliki wapaswa kufanya nini wakati mmoja wa Mashahidi wa Yehova anapozuru nyumbani mwao? Kichapo cha juzijuzi kilichotayarishwa na baraza la National Catechistic Bureau of the Italian Bishops’ Conference chataarifu hivi: “Kukataa mazungumzo, kwa fadhili lakini hata hivyo kwa uthabiti, si ukosefu wa fadhili.”

Si Wakatoliki wote wanaoafiki, kama ionyeshwavyo na barua liliyopelekewa gazeti la kila siku la Gazzetta del Mezzogiorno na mtu anayeishi katika Foggia, Italia:

“Mimi si mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Mimi ni Mkatoliki. Lakini ninashangazwa na sheria ambazo kanisa hulazimisha waumini, likiwaambia wabandike notisi milangoni mwao za kuwafukuza Mashahidi wa Yehova. Hata hivyo, watu hawa wanahubiri tu Neno la Mungu, na wao husaidia wengine kupata ujuzi wa Biblia wenye kina zaidi. Maagizo hayo juu ya jinsi ya kuepuka Mashahidi wa Yehova hunikumbusha wakati Italia ilipotaabishwa na kipindupindu na tulishauriwa jinsi ya kuepukana na maambukizo.

“Kwa maoni yangu, hilo laonyesha kwamba kanisa hulazimisha sheria zayo bila kujali matamanio ya waumini. Lakini kwa miaka kadhaa sasa, nimeona kwamba hata Wakatoliki wanakwenda kutoka nyumba hadi nyumba, wakizuru nyumba za Mashahidi wa Yehova pia; nao huwaruhusu kuingia, wakizungumza pamoja nao, bila kukataa yeyote.”

Mashahidi wa Yehova hawalazimishi watu kukubali ujumbe wao. Badala ya hivyo, wao hujitahidi kushiriki pamoja na wengine tumaini linalotolewa na Neno la Mungu ambalo wao wenyewe wamelipata kuwa lenye kufariji katika nyakati hizi zenye masumbufu. Kwa kwenda nyumba hadi nyumba, na vilevile kwa kusema na wale wanaokutana nao barabarani, Mashahidi wa Yehova hushiriki habari njema ya Ufalme wa Mungu pamoja na wale walio tayari kusikiliza.—Mathayo 24:14; Matendo 5:42; 17:17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki