Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 9/15 uku. 32
  • Waweza Kutegemea Ahadi za Nani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Waweza Kutegemea Ahadi za Nani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 9/15 uku. 32

Waweza Kutegemea Ahadi za Nani?

MWAKA wa 1893 kikundi cha watalaamu 74 wa kijamii kilikutana kwenye maonyesho ya Chicago World’s Fair ili kuzungumza juu ya wakati ujao. (Mahali pa maonyesho hayo panaonyeshwa juu.) Wakitazama miaka 100 mbele kufikia 1993, miongoni mwa matabiri mengine, walitabiri ifuatavyo: “Urefu wa maisha ya watu wengi utakuwa miaka 150.” “Magereza yatapungua na talaka haitafikiriwa kuwa ya lazima.” “Mfumo wa kiserikali utakuwa sahili zaidi, kwa kuwa ukuu wa kweli sikuzote hutegemea usahili.”

Vivyo hivyo, mwaka wa 1967 kitabu chenye kichwa The Year 2000 kilitabiri hivi: “Kufikia mwaka wa 2000, yaelekea kompyuta zitakuwa sawa na, ziige, au kuzidi baadhi ya uwezo mbalimbali wa kiakili wa wanadamu, ulio ‘kama wa kibinadamu’ zaidi, labda kutia na uwezo wake wa usanii na ubuni.” “Lile wazo la roboti za bei nafuu kufanya nyingi za kazi za nyumbani . . . laonekana kuwa jambo rahisi zaidi kufikia mwaka wa 2000.”

Kutoweza kwa mwanadamu kuona kimbele matukio ya wakati ujao kwatofautiana kwa njia yenye kutokeza na uwezo wa Mungu. Kwa kielelezo, linganisha matabiri yaliyotangulia kutajwa na yale ambayo Biblia ilitabiri karibu karne 20 zilizopita kwa habari ya siku yetu: “Watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wapenda-fedha, wenye kujitanguliza, wenye kiburi, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio waaminifu-washikamanifu, wasio na shauku ya kiasili, wasiotaka upatano wowote, wachongezi, wasio na hali ya kujidhibiti, wakali, wasio na upendo wa wema, wasaliti, wenye vichwa vigumu, wenye kututumuka kwa kiburi, wenye kuzipenda raha badala ya kuwa wapenda-Mungu, wakiwa na namna ya ujitoaji-kimungu lakini wakithibitika kuwa si kweli kwa nguvu ya hiyo.”—2 Timotheo 3:1-5.

Unabii huu wa Biblia kuhusu “siku za mwisho” ni mmoja tu kati ya unabii mwingi ambao umetimizwa siku yetu. Neno la Mungu lilitabiri kwamba “ishara” ya kuwapo kwa Yesu ingetia ndani vita ya ulimwengu, upungufu wa chakula, magonjwa ya kuambukiza, matetemeko ya dunia, na kuhubiriwa kwa habari njema ya Ufalme wa Mungu.—Mathayo 24:3-14; Luka 21:11.

Usahihi usiokosea wa ahadi za Mungu ulimsukuma mwandikaji mmoja wa Biblia kutangaza hivi karne nyingi zilizopita: “Halikuwapungukia ninyi hata neno moja katika mambo hayo mema yote aliyoyanena BWANA, Mungu wenu, katika habari zenu; yote yametimia kwenu hapana neno lo lote mlilopungukiwa.”—Yoshua 23:14.

Ndiyo, twaweza kuhakikishiwa kwamba ahadi zote za Mungu zitatimizwa karibuni. Ufalme wa Mungu utakomesha ugonjwa, uhalifu, uraibu wa dawa za kulevya, njaa, na vita—dunia nzima itakuwa paradiso. (Zaburi 37:10, 11, 29; Ufunuo 21:3, 4) Waweza kutumainia utimizo wa unabii huo! Watoka kwa Muumba wetu, “asiyeweza kusema uwongo.”—Tito 1:2; linganisha Waebrania 6:13-19.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Cleveland State University Archive

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki