Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w97 11/15 uku. 32
  • Masiku ya Kukosa Usingizi Yaliyokuwa Yenye Manufaa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Masiku ya Kukosa Usingizi Yaliyokuwa Yenye Manufaa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
w97 11/15 uku. 32

Masiku ya Kukosa Usingizi Yaliyokuwa Yenye Manufaa

HATA wafalme wana masiku ya kukosa usingizi. Karne ya tano K.W.K., mtawala mwenye nguvu wa Uajemi, Ahasuero, alikosa usingizi usiku mmoja. Labda akihisi kwamba alikuwa amepuuza wajibu fulani, aliamuru asomewe rekodi za kifalme. Alipata habari kwamba mtumishi fulani mwaminifu, Mordekai, alikuwa amezuia njama ya mauaji lakini hakuwa amethawabishwa. Ahasuero aliazimia kurekebisha kughafilika huko mara moja. Matokeo yenye manufaa ya matendo yake juu ya watu wa Mungu yaonyesha kwamba kukosa usingizi kwa mfalme kulisababishwa na Mungu.—Esta 6:1-10.

Kutaniko la Mashahidi wa Yehova katika Hermanus, mji ulio mwambao wa Afrika Kusini, lina sababu ya kukumbuka sehemu hii ya Biblia. Walikuwa wakikutana katika jumba lililopangishwa. Kwa miaka mingi walikuwa wamejaribu kununua rasilimali ili wajenge Jumba la Ufalme lao wenyewe. Hatimaye, mwaka wa 1991, uwanja mzuri sana ulitolewa na Halmashauri ya Mji.

Hata hivyo, watu fulani walipinga uuzaji wa uwanja huo kwa Mashahidi wa Yehova. Baada ya kukawia kwa miezi kadhaa, hilo kutaniko lilijulishwa kwamba ruhusa ya kuyauzia makanisa rasilimali ilikuwa imekawizwa kwa miaka mitatu na nusu, na lile toleo la uwanja likaondolewa. Mei 1993 hilo kutaniko liliandika barua tena, likiomba hiyo halmashauri ifikirie tena uamuzi wake. Kwa kujibiwa walipokea barua yenye sentensi moja, ikitaarifu kwamba ruhusa ya kukawiza uuzaji ilikuwa bado yatumika.

Oktoba mwaka huo, mmojawapo wa madiwani wa mji alikosa usingizi usiku. Alitumia huo wakati akifungua-fungua kurasa za kumbukumbu za zamani za mikutano ya halmashauri kuona ikiwa mambo yoyote yalihitaji uangalifu. Barua iliyoandikwa na Mashahidi wakiomba hiyo halmashauri ifikirie uamuzi wake ilivuta uangalifu wake. Hivyo aliamua kuweka jambo hilo katika ajenda ya mkutano uliofuata. Alitaka kuonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa wamepeleka ombi la uwanja kabla ruhusa ya kukawiza uuzaji wa rasilimali kwa makanisa haijatolewa.

Kwa wakati upasao hilo kutaniko liligawiwa rasilimali hiyohiyo iliyokuwa imetolewa kwao hapo awali mwaka wa 1991! Hiyo rasilimali iko kwenye barabara kuu, mahali ambapo washiriki wa kutaniko na wenye kupendezwa waweza kufika kwa urahisi. Wamejenga Jumba la Ufalme zuri, ambalo liliwekwa wakfu kwa Yehova Oktoba 5, 1996.

Ingawa kutaniko lajutia kule kusumbuka kwa diwani kwa kukosa usingizi usiku, huenda akaliwazwa na uhakika wa kwamba hata Mfalme Ahasuero alikosa usingizi usiku mmoja. Na katika visa vyote viwili matokeo yalikuwa yenye manufaa. Kwa hakika kutaniko lililoko Hermanus lashukuru sana kuwa na Jumba la Ufalme lake lenyewe, kitovu cha ibada safi na mazoezi ya kitheokrasi katika mji huo wa mwambao wenye kupendwa na wengi.—Waebrania 10:24, 25.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki