Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 1/1 uku. 29
  • ‘Fanyeni Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Fanyeni Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 1/1 uku. 29

‘Fanyeni Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’

“KWA hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu.” Hivyo ndivyo Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo itafsirivyo amri ya Yesu kwenye Mathayo 28:19. Hata hivyo, tafsiri hiyo imechambuliwa. Kwa kielelezo, kijitabu kimoja cha kidini chadai hivi: “Tafsiri pekee iruhusiwayo na maandishi ya Kigiriki ni: ‘Fanyeni mataifa yote kuwa wanafunzi!’” Je, hilo ni kweli?

Tafsiri hii, “Fanyeni mataifa yote kuwa wanafunzi,” huonekana katika tafsiri nyingi za Biblia nayo ni tafsiri sisisi kutoka katika Kigiriki. Kwa hiyo, kuna msingi gani wa tafsiri, ‘Fanyeni wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza’? Muktadha. Usemi “kuwabatiza” kwa wazi warejezea watu mmoja-mmoja, si mataifa. Msomi Mjerumani Hans Bruns ataarifu hivi: “[Kiambishi] ‘-wa-’ [katika neno ‘kuwabatiza’] hakirejezei mataifa (Kigiriki chafanyiza tofauti iliyo wazi), bali charejezea watu katika mataifa.”

Zaidi, njia ambayo amri ya Yesu ilitekelezwa yapasa kufikiriwa. Kuhusu huduma ya Paulo na Barnaba huko Derbe, jiji katika Asia Ndogo, twasoma hivi: “Baada ya kutangaza habari njema kwa jiji hilo na kufanya wanafunzi wengi, wakarudi Listra na Ikoniamu na Antiokia.” (Matendo 14:21) Ona kwamba Paulo na Barnaba walifanya wanafunzi kutoka kwa baadhi ya watu wa Derbe, wala si jiji lote la Derbe.

Vivyo hivyo, kuhusu wakati wa mwisho, kitabu cha Ufunuo kilitabiri kwamba, si mataifa mazima-mazima yangemtumikia Mungu, bali “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha” ndio ungefanya hivyo. (Ufunuo 7:9) Hivyo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yatetewa kuwa tafsiri yenye kutegemeka ya ‘Andiko lote, lililopuliziwa na Mungu.’—2 Timotheo 3:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki