Jibu Lenye Kuvutia
GAZETI la habari la Katoliki ya Kiroma la Uingereza, Catholic Herald, majuzi lilichapisha barua ifuatayo kutoka kwa msomaji fulani katika Wales: “Usiku mmoja, Mashahidi wa Yehova wawili walinitembelea. Niliweza kusema kwamba Kanisa Katoliki ndilo lililodhamini uasilia wa Agano Jipya walilonukuu. Kwa kunishangaza, mmoja wao alikubali. ‘Ndiyo,’ akasema, ‘mwaudhamini uasilia wa Biblia lakini hamwifuati. Yesu alisema, “mpendane kama vile nimewapenda nyinyi,” lakini mwauana. Katika vita ya mwisho, Wakatoliki waliwaua Wakatoliki, lakini hakuna Shahidi wa Yehova yeyote aliyemwua Shahidi [mwenzake].’ Ningefanya nini ila kukubali tu? Twawezaje kuomba tuwe na muungano na ‘ndugu zetu wasio Wakatoliki’ ilhali hakuna muungano halisi miongoni mwetu wenyewe? Je, hatupaswi kurekebisha kashfa hiyo kwanza?”—Yohana 15:12.
Vile vita viwili vya ulimwengu vya karne hii ya 20 vilianzia katika Jumuiya ya Wakristo na viliua watu wapatao milioni 50 hadi milioni 60. Ingawa hivyo, yaweza kusemwa kikweli kwamba Mashahidi wa Yehova hawakushiriki hata kidogo katika vita hivyo, wala hawahusiki katika mapambano yoyote yanayotukia sasa. Hilo lawezekanaje? Ni juu yako mwenyewe kupata habari zaidi juu ya vifungo vyenye nguvu vya upendo wa Kikristo na juu ya muungano walio nao Mashahidi wa Yehova zaidi ya milioni tano ulimwenguni pote.—Linganisha Isaya 2:4.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
Picha ya U.S. National Archives