Mkusanyiko “Usio wa Kawaida” Wasifiwa
MTANGAZAJI wa redio katika Lima, Peru, aliwashuku sana Mashahidi wa Yehova. Hata hivyo, baada ya kuhudhuria mmoja wa mikusanyiko yao ya wilaya, mtazamo wake ulibadilika kwa njia yenye kutazamisha. Kwa hakika, alivutiwa sana hivi kwamba aliwatolea wasikilizaji wake wa redio maelezo ya kuwapendelea Mashahidi wa Yehova. Yafuatayo ni madondoo ya yale aliyosema:
“Kwa wazi huo mkusanyiko ulikuwa usio wa kawaida. Hakukuwa na kipande chochote cha karatasi sakafuni wala mchuuzi karibu. Hakukuwa na misongamano ya magari. Watu 5,200 walijilipia nauli zao wenyewe za kwenda kwenye stediamu, kila mmoja akiwa na ndoo, kitambara, dasta, kizolea-taka, ufagio, burashi ngumu, glavu, na sabuni ya kuosha na kusugua hapo mahali. Mahali ambapo rangi ilihitajiwa, walipaka rangi. Na fedha hizo zilitoka wapi? Walizichanga wenyewe! Waarifiwapo juu ya jambo lihitajiwalo kufanywa, wote hutoa fedha kwa utayari. Nakwambia, Kanisa Katoliki lalala usingizi kwa habari ya mambo hayo. Nataka kuwapongeza Mashahidi wa Yehova na waratibu wao wa tukio hilo. Na nataka kuwaambia kwa dhati kabisa, Mungu na awasaidie na kuwabariki nyinyi.”
Katika miji mbalimbali ulimwenguni pote mwaka huu, Mashahidi wa Yehova wataonea shangwe “Njia ya Mungu ya Uhai” Mkusanyiko wa Wilaya. Je, wewe utakuwapo?
[Blabu katika ukurasa wa 32]
“Hakukuwa na kipande chochote cha karatasi sakafuni”