Vita Iliyoharibu Karne ya 19
1914
AKIZUNGUMZA juu ya milenia mpya, Charley Reese, mwandika safu za magazeti ya habari wa The Orlando Sentinel, aliandika hivi: “Ile vita ya mwaka wa 1914-1918 iliyoharibu karne ya 19 haijakwisha bado.” Alimaanisha nini? Alieleza hivi: “Historia haidhibitiwi na tarehe. Karne ya 19 yaani itikadi, makisio, mitazamo, na maadili, haikumalizika Jan[uari] 1, 1901. Iliisha mwaka wa 1914. Huo ndio wakati pia ambapo karne ya 20, kwa maana ileile, ilipoanza. . . .
“Yaelekea kwamba mahitilafiano yote ambayo yametuhangaisha muda wote wa maisha yetu yalitokana na vita hiyo. Karibu matokeo yote ya kiakili na ya kitamaduni ambayo tumepata kuishi nayo yalitokezwa na vita hiyo. . . .
“Nafikiri ilileta madhara hayo kwa sababu ilivunjavunja itikadi ya watu ya kwamba wanadamu wanaweza kuwa na mamlaka juu ya yale yatakayowapata wakati ujao. . . . Vita hiyo iliondolea mbali itikadi hiyo isiyo ya kweli. Hakuna yeyote kutoka pande zote mbili aliyetarajia mambo yawe jinsi yalivyotukia. Iliharibu milki ya Uingereza na ya Ufaransa. Iliua kizazi bora zaidi cha wanaume wa Uingereza, Ufaransa na Ujerumani. . . . Kwa kitambo kidogo tu, iliua watu milioni 11.”
Kwa zaidi ya miaka 120, Mashahidi wa Yehova wameutaja mwaka wa 1914 kuwa mwisho wa aliyoyaita Yesu “nyakati zilizowekwa rasmi za mataifa.” (Luka 21:24) Mwaka huo, Yesu Kristo aliyefufuliwa na kutukuzwa alitawazwa kuwa Mfalme wa Ufalme wa kimbingu. Kupitia Ufalme huo, Yehova Mungu ataondoa mateso yote kabisa ambayo yamekuwa kawaida ya karne hii.—Zaburi 37:10, 11; Mhubiri 8:9; Ufunuo 21:3, 4.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
U.S. National Archives photo