Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 10/15 uku. 32
  • “Sisi Wakatoliki Tuna Mengi ya Kujifunza Kutoka Kwao”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Sisi Wakatoliki Tuna Mengi ya Kujifunza Kutoka Kwao”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 10/15 uku. 32

“Sisi Wakatoliki Tuna Mengi ya Kujifunza Kutoka Kwao”

MWALIMU mmoja katika Bari, Italia, alikuwa na maoni hayo kuhusu Mashahidi wa Yehova, wakati wa somo lake la shule ya upili la historia ya dini. Mwalimu huyo alikuwa ameambia darasa kwamba angetumia vidiokaseti ziwe misaada ya kufundishia. Aliposikia hivyo, mmoja wa wanafunzi mwenye umri wa miaka 18 aitwaye Roberto, alidokeza kutia ndani dini yake kwenye mazungumzo hayo. Alimtolea vidio Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name. Alikubali toleo la Roberto, na darasa zima la wanafunzi 30 waliitazama vidio hiyo. “Wote walivutiwa na muungano, mpango wa kitengenezo, na upendo mwingi uliokuwa miongoni mwa Mashahidi wa Yehova,” asema Roberto. “Hata walishangaa kujua kwamba nakala milioni 40 za Mnara wa Mlinzi na nakala milioni 36 za Amkeni! huchapwa kila mwezi.”

“Sikufikiri kwamba nyinyi mna mpango hivyo,” wakasema baadhi ya wanadarasa wenzi wa Roberto baada ya kuiona vidio hiyo. Kuhusu Mashahidi wa Yehova, mwalimu aliambia darasa: “Oneni jinsi imani yao inavyowachochea wawe na muungano na wenye kupanga mambo kitengenezo. Sisi Wakatoliki tuna mengi zaidi ya kujifunza kutoka kwao.” Vidio hiyo na mazungumzo ya darasa yaliyofuata yalichangia sana kukuza uelewevu mzuri kuhusu Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki