Siku ya Kukumbukwa
Jioni iliyotangulia kifo chake, Yesu alipitisha mkate usiotiwa chachu na kikombe cha divai kwa mitume wake na kuwaagiza wale na kunywa. Pia aliwaambia hivi: “Fulizeni kufanya hili katika ukumbuko wangu.”—Luka 22:19.
Mwaka huu ukumbusho wa tukio hilo utakuwa siku ya Alhamisi, Aprili 1, baada ya mshuko-jua. Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote watakusanyika usiku huu wa pekee ili kuadhimisha Ukumbusho huo kwa njia ambayo Yesu aliamuru. Unakaribishwa kwa uchangamfu ujiunge nasi. Tafadhali pata habari kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu ili upate kujua wakati na mahali barabara pa kufanyia mkutano huu wa pekee.