Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 4/1 uku. 32
  • Wasimamizi Wawasifu Mashahidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasimamizi Wawasifu Mashahidi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 4/1 uku. 32

Wasimamizi Wawasifu Mashahidi

HUKO Cádiz, jiji lenye bandari lililoko [kilometa 500] kusini-magharibi mwa Madrid, Hispania, meya Doña Teófila Martínez aliwatuza Mashahidi wa Yehova kwa bamba la taarifa (linaloonyeshwa juu). Bamba hilo lasema hivi: “Wasimamizi wa jiji la Cádiz watuza Mashahidi wa Yehova kwa sababu ya ushirikiano wao na kwa jitihada zao kwa ajili ya jiji hili.” Mashahidi walifanya nini ili kupata heshima hiyo?

Mashahidi walipata heshima hiyo kutokana na kutambuliwa kwa kazi ambayo walikuwa wamefanya ya kurekebisha sehemu moja ya stediamu ya manispaa ya jiji hilo. Kwa miisho-juma kadhaa, mamia ya Mashahidi walijitolea kusaidia kurekebisha vyoo vya orofa ya chini ya stediamu ya soka ya Carranza. Sasa, wote wanaotumia stediamu hiyo wamenufaika kutokana na mifereji iliyowekwa, mabomba yaliyorekebishwa, na sakafu zilizowekwa.

Kwa muda fulani, Mashahidi wa Yehova wamefurahia uhusiano mzuri pamoja na wasimamizi wa jiji la Cádiz. Kila mwaka, wasimamizi wa jiji hilo huwaruhusu Mashahidi watumie Stediamu ya Carranza kwa ajili ya mkusanyiko wao wa wilaya wa kila mwaka. Kwa hiyo, Mashahidi hufurahi kufanya yote wawezayo ili kusaidia kutunza stediamu hiyo.

Hata hivyo, zaidi ya kazi ngumu ambayo wao hufanya mara kwa mara, Mashahidi wa Yehova huzuru vitongoji vya jiji hilo ili kuunga umma mkono katika njia nyingine. Wao hutangaza “habari njema” ya Ufalme wa Mungu. Bila shaka, wao hawashiriki katika huduma ya umma ili kupata sifa kutoka kwa wanadamu. Wao hufanya hivyo kwa kutii amri ya Yesu ya kuhubiri ‘habari njema ya ufalme’ na ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.’ (Mathayo 24:14; 28:19) Kwa njia hiyo, Mashahidi wa Yehova wanatumaini kutumikia jumuiya kwa kuwaelimisha watu katika “njia ya haki.”—Mithali 12:28.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki