Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 4/15 uku. 32
  • Amani ya Ulimwengu—Kutoka Chanzo Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Amani ya Ulimwengu—Kutoka Chanzo Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 4/15 uku. 32

Amani ya Ulimwengu—Kutoka Chanzo Gani?

JE, KUENEZWA kwa elimu na dini tufeni pote kutaleta amani ya ulimwengu? Huo ndio mradi wa Dakt. Robert Muller, aliyekuwa msaidizi wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa na mpokeaji wa Tuzo la 1989 la Elimu ya Amani la UNESCO. Kama ilivyoripotiwa katika gazeti la habari The Vancouver Sun, Dakt. Muller “anasadiki kwamba ni lazima wanafunzi tufeni pote wafundishwe mambo fulani ya msingi na kanuni zinazohusu sayari, ubinadamu na kutofanya jeuri.” Yeye awazia siku ambapo taasisi za elimu ulimwenguni pote zitafundisha watoto juu ya UM kuwa tumaini bora zaidi la kupata amani. Yeye pia aamini kwamba “dini zote za ulimwengu zapaswa kuwa washiriki wa shirika jipya linalofanana na UM linaloitwa Umoja wa Dini,” gazeti la Sun laripoti. Kisha, “mafundisho yote ya kidini yataendeleza hali ya kutofanya jeuri.”

Je, amani ya ulimwengu itapata kuwa halisi? Bila shaka! Lakini si kupitia shirika lolote la kibinadamu. Zaidi ya miaka 2,700 iliyopita, mwandikaji aliyepuliziwa alitambulisha chanzo kikuu zaidi cha elimu ya kupata amani alipotabiri kwamba watu wenye mioyo minyofu ‘wangefundishwa na BWANA,’ na amani yao ingekuwa “nyingi.”—Isaya 54:13.

Mungu ndiye “apaye amani,” Biblia yasema. (Waroma 16:20) Hata sasa programu ya elimu iliyo bora zaidi inaendelea tufeni pote, Yehova anapofundisha watu wake ‘kutafuta sana amani na kuifuatia,’ ‘kufua panga zao ziwe majembe,’ na ‘kutojifunza vita tena kamwe.’—1 Petro 3:11; Isaya 2:2-4.

Ibada inayotegemea kweli, isiyo na unafiki wala udanganyi, inakubaliwa na kubarikiwa na Mungu. (Mathayo 15:7-9; Yohana 4:23, 24) Ni ibada ya kweli pekee, inayopatana kabisa na Neno la Mungu, iwezayo kutokeza watu ambao huishi kwa amani na umoja na wanaopendana kikweli.—Yohana 13:35.

Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu yale Neno la Mungu lisemayo kuhusu amani ya ulimwengu, twakuomba uwasiliane na wachapishaji wa jarida hili.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki