“Mume Mwenye Furaha wa Mke Anayependeza kwa Wema”
MARA kwa mara, watu fulani huwalaumu Mashahidi wa Yehova waziwazi kuwa wanavunja ndoa. Hata hivyo, ndoa nyingi sana zinazofanikiwa, ambazo mwenzi mmoja tu ndiye Shahidi wa Yehova, zaonyesha kuwa hilo si kweli kabisa. Kutii shauri la Biblia katika maisha ya familia huleta furaha katika ndoa, kama vile barua ifuatayo iliyochapishwa katika gazeti la habari la Ufaransa ionyeshavyo.
“Kwa takriban miaka 28 sasa, nimekuwa mume mwenye furaha wa mke anayependeza kwa wema ambaye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Alilea watoto wangu watano, ambao wawili kati yao si wake mwenyewe, akiwatunza wote kwa njia sawa na kuwaonyesha upendo mwingi. Nikiwa sasa mkurugenzi wa kampuni yenye waajiriwa 45, naweza kuwahakikishia kwamba yeye amechangia sana ufanisi wangu wa kitaaluma. Hiyo ndiyo sababu, nilipoona makala fulani katika gazeti la habari ninalosoma kwa ukawaida ikionyesha Mashahidi wa Yehova kuwa tisho kwa eneo la Lot-et-Garonne, niliamua kuwatolea ushuhuda wenye kuaminika.”
Barua hiyo pia yasema: “Hawavuti sigareti wala hawalewi. Je, hilo ni tisho? Wao ni Wakristo wenye uvumiliano, wasiomlazimisha yeyote afuate sheria wanazofuata. Badala yake, wao ni kielelezo katika njia nyingi. . . . Hawahusiki katika kashfa za kifedha au ulanguzi wa dawa za kulevya. Hawali kiapo cha kutofanya ngono, nami naweza kuwahakikishia kwamba wanaishi maisha ya kawaida. . . .
“Huenda ukaniuliza: Mbona, basi, wewe mwenyewe si Shahidi wa Yehova? Kwa sababu imani ya Kikristo na kushika maadili kabisa kwahitajiwa, na hilo si rahisi kwa watu walio wengi.”