Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 10/1 kur. 16-17
  • Alisaidia Kueneza Nuru “Hadi Ncha ya Dunia”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Alisaidia Kueneza Nuru “Hadi Ncha ya Dunia”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Tulishirikiana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Mfurahieni Yehova na Kushangilia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Yehova Huwavuta Wanyenyekevu Kuijua Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Je, Una Mkazo?
    Amkeni!—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 10/1 kur. 16-17

Alisaidia Kueneza Nuru “Hadi Ncha ya Dunia”

MTUME Paulo alitumiwa kueneza nuru ya kiroho “hadi ncha ya dunia.” Tokeo lilikuwa kwamba wengi “waliokuwa na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele wakawa waamini.”—Matendo 13:47, 48; Isaya 49:6.

Hamu nyingi ya kueneza nuru ya kiroho ilidhihirika pia katika maisha ya kujitoa na yenye jitihada nyingi za Kikristo ya William Lloyd Barry, mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Ndugu Barry alikufa Julai 2, 1999, alipokuwa akishughulikia sehemu katika mkusanyiko wa wilaya huko Hawaii.

Lloyd Barry alizaliwa huko New Zealand Desemba 20, 1916. Mama na baba yake walipendezwa sana na kweli za Biblia zilizokuwa katika vichapo vya C. T. Russell, zilizogawanywa na Watch Tower Bible and Tract Society. Hivyo, Ndugu Barry alilelewa katika familia ya Kikristo yenye kujitoa.

Ingawa alipendezwa sana na michezo na elimu, hata akapata shahada ya digrii katika sayansi, Ndugu Barry alidumisha hamu nyingi kwa mambo ya kiroho. Hivyo, Januari 1, 1939, alianza huduma ya wakati wote na kuwa mshiriki wa familia ya Betheli kwenye ofisi ya Sosaiti huko Australia. Baada ya serikali kuipiga marufuku Sosaiti mwaka 1941, Ndugu Barry aliendelea kushughulika sana na kazi ya ofisi, nyakati nyingine akipewa mgawo wa kuandika habari za kuwatia moyo waamini wenzake. Aliweka kielelezo kizuri pia katika huduma ya shambani.

Katika Februari 1942, Ndugu Barry alioa mtumishi mwingine wa wakati wote. Mke wake mpendwa, Melba, amefanya kazi pamoja naye kwa miaka hii yote katika sehemu nyingi za dunia. Walipiga hatua kubwa ya kutumikia katika maeneo ya kigeni kwa kuhudhuria darasa la 11 la Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower nchini Marekani. Walipewa mgawo wa kwenda katika nchi ambayo wengi wangeifikiria kuwa “ncha ya dunia”—Japani. Baada ya kuwasili huko katika Novemba 1949, walianza kutumikia wakiwa wamishonari katika jiji lenye bandari la Kobe. Wakati huo, watu 12 tu ndio waliokuwa wakihubiri habari njema nchini Japani. Ndugu Barry alijifunza lugha na desturi za nchi hiyo mpya, akawapenda sana watu wa Japani, ambao alitumikia pamoja nao kwa miaka 25 iliyofuata. Upendo wake kwa wale “waliokuwa na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele” ulikuwa wazi kwa ndugu Wakristo wenye kuongezeka nchini Japani, ukimsaidia kuwa msimamizi afaaye wa ofisi ya tawi kwa miongo mingi.

Katikati ya mwaka wa 1975, Japani ilipokuwa na Mashahidi wapatao 30,000, Ndugu Barry na mke wake walihamishwa kwenda Brooklyn, New York. Akiwa Mkristo mtiwa-mafuta kwa roho, Ndugu Barry alikuwa amealikwa atumikie akiwa mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. (Waroma 8:16, 17) Uzoefu wake wa kuandika ulifaa sana kwa kazi yake mpya katika Idara ya Uandikaji. Nao uzoefu mwingi aliopata akitumikia katika ofisi ya tawi na pia wa kimataifa ulimtayarisha kutimiza fungu muhimu akiwa mshiriki wa Halmashauri ya Utangazaji ya Baraza Linaloongoza.

Kwa miaka ambayo imepita, Ndugu Barry aliendelea kupenda eneo la Mashariki na watu wake. Wanafunzi katika Shule ya Gileadi na pia washiriki wa familia ya Betheli walijua kwamba hotuba na maelezo yake yangekazia masimulizi yenye kutia moyo juu ya wengi waliotumikia katika kazi ya umishonari. Shughuli za kuhubiri Ufalme katika ‘ncha za dunia’ zilisisimua kwelikweli Ndugu Barry aliposimulia kwa shauku mambo aliyojionea. Baadhi ya masimulizi hayo yametajwa katika simulizi lake binafsi lililochapishwa katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 1960, (la Kiingereza).

Tuna hakika kwamba akiwa ‘mrithi-mshirika pamoja na Kristo,’ Ndugu Barry ataendelea kuwapenda wale ‘walio na mwelekeo ufaao kwa ajili ya uhai udumuo milele.’ Bila shaka, atakumbukwa sana na wote waliomjua na kumpenda akiwa mtu wa kiroho, aliyejitoa kabisa kwa Yehova na mwenye kuwapenda sana watu wa Mungu. Lakini tunafurahi kwamba Ndugu Barry alivumilia kwa uaminifu hadi mwisho wa maisha yake ya kidunia.—Ufunuo 2:10.

[Picha katika ukurasa wa 16]

Lloyd Barry na John Barr wakati kichapo “Insight on the Scriptures” kilipotolewa mwaka wa 1988

[Picha katika ukurasa wa 16]

Waliohitimu kwenye darasa la 11 la Gileadi, wakiwa wamekutana huko Japani baada ya miaka 40

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki