Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 11/15 uku. 3
  • Je, Biblia Inaweza Kutusaidia Leo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Biblia Inaweza Kutusaidia Leo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Kitabu Kinachopuuzwa na Vijana Wengi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kunufaika kwa Usomaji wa Biblia Kila Siku
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Kwa Nini Uisome Biblia?
    Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
  • Jinsi Unavyoweza Kunufaika Zaidi Unaposoma Biblia
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 11/15 uku. 3

Je, Biblia Inaweza Kutusaidia Leo?

“ASILIMIA 1 hivi ya Biblia yote nzima ndiyo inayostahili kusomwa, na sehemu zile nyingine hazifai na zimepitwa na wakati.” Hivyo ndivyo mwanamume mmoja kijana alivyosema. Wengi wangekubaliana naye. Ingawa Biblia yaendelea kuwa kitabu kinachouzwa zaidi ulimwenguni kote, mamilioni ya watu hawaisomi nao hawafahamu mafundisho yake.

Toleo la gazeti la habari la Ujerumani Süddeutsche Zeitung la Krismasi ya mwaka wa 1996 lilieleza kwamba “wasomaji wa [Biblia] wanazidi kupungua. Katika enzi ya sayansi na hali inayoenea ya kufuatia mambo yasiyo ya kidini, wengi huyaona masimulizi ya Biblia kuwa mageni na magumu kueleweka.” Uchunguzi mbalimbali wathibitisha jambo hilo. Uchunguzi mwingine waonyesha kwamba watoto wengi hata hawajui kabisa Yesu ni nani. Katika uchunguzi mmoja, watu wanaopungua nusu ya wale waliohojiwa waliweza kusimulia hadithi za Biblia za mwana mpotevu na Msamaria aliyekuwa jirani mwema.

Kichapo Reformiertes Forum cha Kanisa la Kievanjeli la Uswisi chasema kwamba nchini Uswisi Biblia hazinunuliwi sana kama hapo awali. Hata wale walio na Biblia, mara nyingi hiyo hukaa tu kwenye rafu bila kusomwa. Hali iko vivyo hivyo nchini Uingereza. Kwa mujibu wa uchunguzi mmoja, hata ingawa watu wengi wana Biblia, wengi hawaisomi.

Kwa upande mwingine, mamilioni ya watu ulimwenguni kote wana maoni tofauti kuhusu Biblia. Wanaiona kuwa Neno la Mungu na pia kuwa yenye thamani na yenye manufaa. Hivyo, wao huisoma kwa ukawaida. Mwanamke mmoja kijana aliandika: “Mimi hujitahidi kusoma sura moja au mbili za Biblia kila siku. Nafurahia jambo hilo sana.” Watu hao huzingatia sana yale ambayo Biblia hufundisha, nao hujitahidi kutumia mashauri yake maishani mwao. Wanaamini kwamba Biblia inaweza kuwasaidia katika ulimwengu wa leo wenye taabu.

Wewe waonaje? Je, Biblia haifai siku hizi? Au ni yenye thamani na yenye manufaa? Je, Biblia inaweza kutusaidia leo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki