Mwaka Muhimu kwa Ugawanyaji wa Biblia
LEO, watu wengi zaidi kuliko wakati mwingine wowote wana Biblia. Hivyo ndivyo inavyodokeza ripoti moja ya United Bible Societies, kwa maana ugawanyaji wa Biblia mwaka wa 1998 uliongezeka kwa zaidi ya nusu milioni kuliko mwaka uliotangulia. Kwa jumla, Biblia zaidi ya 585,000,000—zikiwa sehemu au zikiwa kamili—ziligawanywa ulimwenguni kote. “Jambo hilo latia moyo,” ripoti hiyo yataarifu. “Neno la Mungu linawafikia watu wengi zaidi leo.”
Pasipo shaka, kuna tofauti kati ya kuwa na Biblia na kuisoma. Kwa kielelezo, uchunguzi mmoja ulionyesha kwamba zaidi ya asilimia 90 ya Wamarekani wana angalau Biblia moja, na idadi sawa na hiyo kati yao wanaamini kuwa Biblia ni chanzo chema cha mafundisho ya maadili. Hata hivyo, ni asilimia 59 peke yao waliosema kuwa wanatafuta shauri katika Biblia. Na asilimia 29 walikiri kwamba “hawaijui sana” Biblia au “hawaijui hata kidogo.”
Mashahidi wa Yehova huchapisha na kugawanya Biblia na vilevile huongoza mafunzo ya Biblia nyumbani bila malipo pamoja na watu katika nchi zaidi ya 230. Mamilioni ya watu ulimwenguni kote sasa wananufaika na mpango huo wa elimu ya Biblia. Wanasaidiwa kukabiliana na matatizo yanayowakumba sasa, nao hujifunza mambo ambayo Biblia yasema kuhusu wakati ujao ulio mzuri chini ya Ufalme wa Mungu.—Isaya 48:17, 18; Mathayo 6:9, 10.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Mafunzo ya Biblia nyumbani katika (kuanzia juu kushoto hadi kulia) Bolivia, Ghana, Sri Lanka, na Uingereza