Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w00 7/15 uku. 32
  • Kazi Njema Zamletea Mungu Sifa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kazi Njema Zamletea Mungu Sifa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
w00 7/15 uku. 32

Kazi Njema Zamletea Mungu Sifa

WANAOMPENDA Mungu wanajaribu kuishi kupatana na nuru ya kiroho ya Neno lake, Biblia. Kwa njia hiyo wanafuata amri ya Yesu: “Acheni nuru yenu ing’ae mbele ya watu, ili wapate kuona kazi zenu bora na kumpa utukufu Baba yenu aliye katika mbingu.” (Mathayo 5:16) Yasemwayo na hali kadhalika mwenendo mwadilifu, zaweza kumletea Mungu sifa.

Mashahidi wa Yehova wanajaribu kumpendeza Mungu kwa kufuata Biblia na kwa kujitahidi kusaidia wengine kiroho. Wanafanya hivyo hata katika nchi ambapo huduma yao haijasajiliwa bado. Katika mji mkuu wa mojawapo ya nchi hizi, Mashahidi wamekuwa na mikusanyiko ya kila mwaka ambayo watu 6,000 hadi 9,000 wamehudhuria. Kwa ajili ya mikusanyiko hiyo, wamekodi majumba katika jengo la maonyesho. Sawa na jinsi walivyokuwa wakifanya miaka iliyotangulia, kabla ya mkusanyiko wao wa mwaka wa 1999, mamia ya Mashahidi walifanya kazi kwa bidii kusafisha jengo hilo na kuweka mfumo wa sauti na maelfu ya viti.

Matayarisho hayo yote yalikuja kujulikana. Wasimamizi wa jengo hilo waliangalia kwa makini utendaji huo. Waliona ya kwamba, ijapokuwa watu 15,666 walihudhuria, mambo yote yalitendeka bila taabu na kwamba Mashahidi walikuwa wenye utaratibu sana. Wasimamizi hao walivutiwa pia na jinsi jengo lilivyosafishwa kabisa baada ya mkusanyiko.

Wasimamizi walionyesha uthamini wao kwa kuwapa Mashahidi haki ya kutangulia kukodi jengo hilo mwaka uliofuata. Lakini wasimamizi hao walifanya hata zaidi. Mnamo Julai 15, 1999, waliwapa ndugu waliosimamia mkusanyiko zawadi. Maandishi yaliyochongwa katika bamba walilopewa yasema “kutaniko la Mashahidi wa Yehova”—jambo lisilotazamiwa katika nchi ambapo kazi yao ya kufundisha Biblia imezuiliwa.

Ulimwenguni pote katika mwaka wa 2000 na 2001, mamilioni ya watu watahudhuria mamia ya Mikusanyiko ya Wilaya ya Mashahidi wa Yehova yenye kichwa “Watekelezaji wa Neno la Mungu.” Ikiwa utakuwapo, wewe mwenyewe waweza kuona jinsi wale wanaotenda kwa kupatana na Biblia wanavyofanya kazi njema zinazomletea Mungu sifa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki