Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w00 8/15 uku. 32
  • Somo Kutokana na Baharia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Somo Kutokana na Baharia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
w00 8/15 uku. 32

Somo Kutokana na Baharia

KUSAFIRI kwa mashua ukiwa peke yako kwenye bahari kuu kunaweza kuchosha sana. Athari ya uchovu yaweza kumhatarisha baharia kwa urahisi, na hivyo basi kusababisha makosa na kufanya maamuzi mabaya. Kwa sababu hiyo, yeye anathamini sana nanga. Nanga humwezesha baharia ambaye amechoka kupumzika na kupata nguvu tena bila hatari ya kupeperushwa. Wakati huohuo, nanga hulazimisha omo kukabili upepo na mawimbi na hivyo kufanya mashua iwe imara zaidi.

Sawa na vile mabaharia hukabili hatari nyingi baharini, ndivyo Wakristo wanavyokabili mikazo ya daima ya ulimwengu huu na wanahisi uhitaji wa pumziko. Hata Yesu wakati mmoja aliwapendekezea hivi wanafunzi wake: “Njoni, nyinyi wenyewe, kwa faragha mwingie katika mahali pa upweke mpumzike kidogo.” (Marko 6:31) Leo wengine huchukua likizo ya majuma machache au mwisho-juma ili kupumzika pamoja na familia zao. Pindi hizo zinaweza kuwa zenye kuburudisha na kututia nguvu tena. Tunaweza kuhakikishaje kwamba tuko salama kiroho katika pindi kama hizo? Ni nini ambacho chaweza kutumika kama nanga yetu ya kiroho ambacho kitatusaidia tusipeperushwe na kutufanya tuwe imara?

Kwa ukarimu Yehova ametufanyia uandalizi. Uandalizi huo ni Neno lake Takatifu, Biblia. Tukiisoma kila siku, tutakuwa karibu na Yehova na kamwe hatutapeperushwa tutoke kwake. Mashauri yake yanaweza kutuimarisha na kutuwezesha kukinza vishawishi vya Shetani na ulimwengu wake. Kudumisha kwetu programu ya kusoma Biblia kwa ukawaida, hata wakati ambao hatukuratibu kuisoma, kunaweza kuwa nanga yetu ya kiroho.—Yoshua 1:7, 8; Wakolosai 2:7.

Mtunga-zaburi atukumbusha kwamba “heri [“mwenye furaha,” NW] mtu yule” ambaye “sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, na sheria yake huitafakari mchana na usiku.” (Zaburi 1:1, 2) Kusoma Neno la Mungu kila siku kutatupatia “furaha” ya kuburudishwa na kutiwa nguvu, tukiwa tayari kuendelea katika mwendo wetu wa Kikristo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki