Upendo wa Kikristo Ni Zaidi ya Maneno Tu
MOTO ulipoteketeza makao ya familia ya Bartholomew huko Trinidad, walipoteza vitu vyao vyote isipokuwa uhai wao. Mtu fulani wa ukoo mwenye kuishi karibu aliwakaribisha kwake, lakini hilo halikuwa mwisho wa tukio hilo.
Olive Bartholomew ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova, nao washiriki wa kutaniko lake—kutia ndani makutaniko ya eneo la karibu—walianza kutoa michango ya kutumiwa kujenga upya nyumba ambayo yeye na washiriki wengine wa familia yake walikuwa wamepoteza. Halmashauri iliundwa ili kuendesha mradi huo, na ujenzi ukaanza. Mashahidi wapatao 20, pamoja na majirani kadhaa walikuwepo kwenye ujenzi huo. Hata vijana walijiunga na kazi, watu wengine nao wakaleta viburudisho.
“Washiriki wa familia yangu wamevutiwa sana,” akasema Olive, kama ilivyoripotiwa na gazeti Sunday Guardian la Trinidad. “Wao si Mashahidi, na mume wangu bado ameduwaa kutokana na yale anayoyaona.”
Akitoa muhtasari wa jitihada hiyo, mratibu wa mradi huo wa ujenzi alikazia kuwa matendo ya aina hiyo kwa kweli ni alama za kutambulisha Ukristo wa kweli. “Sisi hatuendi tu nyumba hadi nyumba tukisema juu ya upendo,” yeye akasema. “Bali tunajaribu kutenda yale tunayohubiri.”—Yohana 13:34, 35.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Olive Bartholomew akiwa pamoja na mume wake