“Kielelezo cha Muungano”
HICHO kilikuwa kichwa cha tahariri iliyochapishwa katika gazeti moja huko Indaiatuba, São Paulo, Brazili. Ni nani walioweka kielelezo hicho? “Mashahidi wa Yehova wanaopanga kujenga ‘Jumba la Ufalme’ jipya, kama yaitwavyo mahekalu au majumba yao, wanaweka kielelezo halisi kinachoweza kuigwa cha ushirikiano usioweza kupuuzwa,” akaeleza mwandishi huyo.
Muungano uliopo miongoni mwa Mashahidi wa Yehova huonekana katika pindi kama hizo. Hivyo, makala hiyo ilisema hivi: “Inavutia kuona wanaume, wanawake na matineja waliojitolea kufanya kazi pamoja ili kujenga mahali pa kukutania na kumwabudu Mungu.”
Mashahidi wa Yehova ni vielelezo vizuri katika mambo mengine pia. “Mbali na kujifunza na kusali, lengo lao ni kusaidia waraibu wa vileo na wa dawa za kulevya waishi maisha ya kawaida na kuonyesha watu njia ya muungano na upendo,” ikaongezea tahariri hiyo. Wanapataje muungano huo? Mashahidi wanajua kwamba kujifunza na kutumia shauri la Biblia husaidia mtu aache mazoea mabaya. Ndiyo sababu wanajitahidi kufundisha wengine yale waliyojifunza kutoka kwa Biblia. Tahariri hiyo yafikia mkataa kwamba “kielelezo chao bila shaka chapasa kuigwa kwa hima.”
Watu wote wanakaribishwa kwenye mikutano ya Mashahidi wa Yehova na hakuna michango inayokusanywa. Unaalikwa kwa uchangamfu kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu nawe.