Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 5/15 uku. 27
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Hekalu Kubwa la Kiroho la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Thamini Pendeleo Lako la Kuabudu Katika Hekalu la Kiroho la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Kumtambua Masihi, Yule Mfalme
    “Ufalme Wako Uje”
  • “Nyumba ya Sala kwa Mataifa Yote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 5/15 uku. 27

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

“Mahali patakatifu kabisa” palitiwa mafuta lini, kulingana na unabii wa Danieli 9:24, BHN?

Danieli 9:24-27 ni unabii kuhusu kutokea kwa “masihi aliye mkuu”—Kristo. Kwa hiyo, kule kutia mafuta “mahali patakatifu kabisa,” hakurejezei kutia mafuta sehemu ya ndani ya Mahali Patakatifu Kabisa katika hekalu la Yerusalemu. Badala yake, usemi “mahali patakatifu kabisa” hurejezea patakatifu pa kimbingu pa Mungu—Patakatifu Zaidi Sana pa Kimbingu—katika hekalu kubwa la kiroho la Yehova.a—Waebrania 8:1-5; 9:2-10, 23.

Hekalu la kiroho la Mungu lilianza kufanya kazi lini? Fikiria kilichotukia wakati Yesu alipobatizwa katika mwaka wa 29 W.K. Tangu ubatizo wake Yesu alitimiza maneno ya Zaburi 40:6-8. Baadaye, mtume Paulo alionyesha kwamba Yesu alikuwa amesali hivi kwa Mungu: “Dhabihu na toleo hukutaka, bali ulinitayarishia mwili.” (Waebrania 10:5) Yesu alijua kwamba Mungu ‘hakutaka’ watu waendelee kutoa dhabihu za wanyama kwenye hekalu la Yerusalemu. Badala yake, Yehova alikuwa amemtayarishia Yesu mwili mkamilifu wa kibinadamu ili autoe kama dhabihu. Yesu alionyesha tamaa ya moyoni mwake kwa kusema: “Tazama! Nimekuja (katika kikuto cha kitabu imeandikwa juu yangu) ili kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.” (Waebrania 10:7) Yehova alionaje jambo hilo? Injili ya Mathayo inasema hivi: “Baada ya kubatizwa mara Yesu akapanda kutoka katika maji; na, tazama! mbingu zikafunguliwa, naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikija juu yake. Tazama! Pia, kulikuwa na sauti kutoka katika mbingu iliyosema: “Huyu ni Mwana wangu, mpendwa, ambaye nimemkubali.”—Mathayo 3:16, 17.

Madhabahu kubwa kuliko ile madhabahu ya hekalu la Yerusalemu ilianza kutumika wakati Yehova Mungu alipokubali mwili wa Yesu kuwa dhabihu. Madhabahu hiyo ilikuwa “mapenzi” ya Mungu, au mpango wake wa kukubali uhai wa kibinadamu wa Yesu kama dhabihu. (Waebrania 10:10) Yesu alipotiwa mafuta kwa roho takatifu ilimaanisha kwamba Mungu alikuwa ameanzisha mpango wake wa hekalu la kiroho.b Kwa hiyo, Yesu alipobatizwa, makao ya kimbingu ya Mungu yalitiwa mafuta, au kutengwa, yawe “mahali patakatifu kabisa” katika mpango wa hekalu kubwa la kiroho.

[Maswali ya Funzo]

a Kwa habari zaidi kuhusu mambo mbalimbali ya hekalu la kiroho la Mungu soma ukurasa wa 14-19 katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Julai 1, 1996.

b Jambo hilo lilirejezewa kwenye ukurasa wa 195 katika kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli!

[Picha katika ukurasa wa 27]

“Mahali patakatifu kabisa” palitiwa mafuta Yesu alipobatizwa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki