Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 8/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Yehova Amwahidi Danieli Thawabu ya Ajabu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Danieli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Jinsi Kitabu Cha Danieli Kinavyokuhusu
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
  • Watahiniwa—Lakini Wadumisha Uaminifu Kwa Yehova!
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 8/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Danieli alikuwa wapi wakati Waebrania watatu walipojaribiwa mbele ya sanamu kubwa iliyosimamishwa na Nebukadneza kwenye uwanda wa Dura?

Biblia haisemi alikuwa wapi, kwa hiyo leo hakuna mtu awezaye kusema kwa uhakika Danieli alikuwa wapi wakati wa jaribu hilo.

Watu wengine wamedokeza kwamba cheo cha Danieli serikalini au mapendeleo ya pekee aliyopewa na Nebukadneza yalikuwa ya juu kuliko ya Shadraka, Meshaki, na Abednego, kwa hiyo Danieli hakuhitajika kwenda kwenye uwanda wa Dura. Andiko la Danieli 2:49 linaonyesha kwamba kwa muda fulani yeye alikuwa na cheo cha juu kuliko wenzake watatu. Lakini hatuwezi kuthibitisha kwamba jambo hilo ndilo lililofanya asihitajike kukusanyika na wengine mbele ya ile sanamu.

Wakijaribu kueleza ni kwa nini Danieli hakuwepo, watu wengine wamesema kwamba huenda alikuwa ameenda kufanya kazi fulani ya kiserikali au alikuwa mgonjwa na hivyo hakuweza kuhudhuria. Lakini Biblia haisemi hivyo. Kwa vyovyote, Danieli alikuwa na sababu nzuri ya kutokuwepo la sivyo maafisa wa Babiloni wenye wivu wangekuwa na sababu ya kumshtaki. (Danieli 3:8) Kabla na baada ya tukio hilo, Danieli alijithibitisha kuwa mtu mwaminifu, mwenye uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu licha ya magumu aliyokabili. (Danieli 1:8; 5:17; 6:4, 10, 11) Kwa hiyo, ingawa Biblia haisemi ni kwa nini Danieli hakuwepo kwenye uwanda wa Dura, tunaweza kuwa na uhakika kwamba alikuwa mwaminifu kabisa kwa Yehova Mungu.—Ezekieli 14:14; Waebrania 11:33.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki