Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 9/15 uku. 28
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Ibada ya Nani Anayoikubali Mungu?
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • Wakristo Huabudu kwa Roho na Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kwa Nini Tuongozwe na Roho ya Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Kuongozwa na Roho ya Mungu Katika Karne ya Kwanza na Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 9/15 uku. 28

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Inamaanisha nini kumwabudu Yehova “kwa roho”?

Alipokuwa akimtolea ushahidi mwanamke mmoja Msamaria aliyekuwa ameenda kuteka maji kwenye kisima kilichokuwa karibu na jiji la Sikari, Yesu Kristo alisema hivi: “Mungu ni Roho, na wale wanaomwabudu yeye lazima waabudu kwa roho na kweli.” (Yohana 4:24) Lazima ibada ya kweli itolewe ‘kwa kweli’ katika maana ya kwamba inapaswa ipatane na yale ambayo Yehova Mungu amefunua katika Biblia juu yake mwenyewe na makusudi yake. Pia ibada yetu kwa Mungu yapasa kutolewa kwa roho katika maana ya kuwa wenye bidii na wenye kuchochewa na moyo uliojaa upendo na imani. (Tito 2:14) Hata hivyo, muktadha unaonyesha kwamba maneno ya Yesu kuhusu ‘kumwabudu Mungu kwa roho’ yahusisha mengi zaidi ya mtazamo wa akili tunaokuwa nao tunapomtumikia Yehova.

Mazungumzo ya Yesu na yule mwanamke kwenye kisima hayakuhusisha kuwa na bidii au kutokuwa nayo katika ibada. Hata ibada isiyo ya kweli inaweza kutolewa kwa bidii na uaminifu. Badala yake, baada ya kusema kwamba Baba hangeabudiwa kwenye mlima huko Samaria au kwenye hekalu huko Yerusalemu, Yesu alitaja njia mpya ya ibada inayotegemea utu halisi wa Mungu. (Yohana 4:21) Alisema: “Mungu ni Roho.” (Yohana 4:24) Mungu wa kweli hana mwili wa nyama na hawezi kuonekana wala kuguswa. Ibada yake haihusishi hekalu au mlima halisi. Kwa hiyo, Yesu alirejezea ibada inayotegemea vitu visivyoonekana.

Mbali na kuabudu kwa kweli, ibada inayokubalika inapasa iongozwe na roho takatifu—kani ya Mungu ya utendaji isiyoonekana. “Roho [takatifu] huchunguza ndani ya mambo yote,” akaandika mtume Paulo, “hata mambo yenye kina kirefu ya Mungu.” Aliongezea hivi: “Sisi tulipokea, si roho ya ulimwengu, bali roho itokayo kwa Mungu, ili tupate kuyajua mambo ambayo tumepewa kwa fadhili na Mungu.” (1 Wakorintho 2:8-12) Ili tumwabudu Mungu kwa njia inayokubalika, lazima tuwe na roho yake na tuongozwe nayo. Isitoshe, ni muhimu kwamba mtazamo wetu wa akili upatane na roho ya Mungu kupitia kujifunza na kutumia Neno lake.

[Picha katika ukurasa wa 28]

Mwabudu Mungu “kwa roho na kweli”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki