Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w02 10/1 uku. 32
  • Je, Wapaswa Kuwa Mtu Asiyejali Sana Mambo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wapaswa Kuwa Mtu Asiyejali Sana Mambo?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
w02 10/1 uku. 32

Je, Wapaswa Kuwa Mtu Asiyejali Sana Mambo?

NAELEKEA watu wengi wangeona kwamba wanapata sifa kwa kuonwa kuwa watulivu, wapole, na wavumilivu. Hata hivyo, mara nyingi mtu mwenye sifa hizo anaweza kuonwa kuwa asiyejali sana mambo. Biblia inasema: “Kutojali kwa wajinga kutawaangamiza.” (Mithali 1:32, NW) Maneno hayo yanamaanisha nini?

Biblia nyingine hutafsiri neno la awali la Kiebrania kuwa “kustarehe bila kujali.” (American Standard Version) Kwa hiyo, kutojali kunahusianishwa na uzembe na kutokuwa mwangalifu na hivyo na ujinga au upumbavu.

Katika karne ya kwanza, Wakristo katika kutaniko la Laodikia hawakujali udhaifu wao wa kiroho. Walijigamba kwamba ‘hawakuhitaji kitu chochote hata kidogo.’ Yesu Kristo aliwasahihisha, akawaonyesha uhitaji wa kuchochea tena bidii yao ya Kikristo.—Ufunuo 3:14-19.

Watu wa siku za Noa pia hawakujali. Walijishughulisha sana na mambo ya kimwili, ‘kula na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiozwa, nao hawakujali mpaka furiko likaja na kuwafagilia mbali wote.’ Kisha Yesu akaongeza kusema: “Ndivyo kuwapo kwa Mwana wa binadamu kutakavyokuwa.”—Mathayo 24:37-39.

Unabii wa Biblia uliotimizwa unaonyesha kwamba tunaishi wakati wa “kuwapo kwa Mwana wa binadamu,” Yesu Kristo. Na tusiwe kamwe watu wasiojali.—Luka 21:29-36.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki