Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w03 10/15 uku. 32
  • “Msiwe Wenye Kufungwa Nira Isiyosawazika”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Msiwe Wenye Kufungwa Nira Isiyosawazika”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
w03 10/15 uku. 32

“Msiwe Wenye Kufungwa Nira Isiyosawazika”

KAMA unavyoona katika picha hii, ngamia na ng’ombe wanalima pamoja kwa shida kubwa sana. Nira inayowaunganisha pamoja—ambayo inakusudiwa kutumiwa na wanyama wawili wenye ukubwa na nguvu sawa—inawaumiza wanyama wote wawili. Kwa kuwajali wanyama hao wa kuvuta mizigo, Mungu aliwaambia hivi Waisraeli, “Usilime kwa ng’ombe na punda wakikokota jembe pamoja.” (Kumbukumbu la Torati 22:10) Kanuni hiyohiyo inaweza kutumiwa pia kuhusu ng’ombe na ngamia.

Kwa kawaida, mkulima hangewatesa wanyama wake kwa njia hiyo. Lakini kama hangekuwa na ng’ombe wawili, angeweza kufunga pamoja wanyama wowote wawili aliokuwa nao. Yaonekana, hivyo ndivyo mkulima wa karne ya 19 kwenye picha hii alivyoamua kufanya. Kwa sababu ya tofauti ya ukubwa na uzito kati ya wanyama hao wawili, mnyama asiye na nguvu nyingi angejitahidi kwenda sambamba na mwenzake, naye aliye na nguvu nyingi angekuwa na mzigo mkubwa zaidi.

Mtume Paulo alitumia mfano wa nira isiyosawazika kutufunza jambo fulani muhimu. “Msiwe wenye kufungwa nira isiyosawazika pamoja na wasio waamini. Kwa maana uadilifu na uasi-sheria vina ushirika gani? Au nuru ina ushiriki gani na giza?” (2 Wakorintho 6:14) Mkristo anawezaje kufungwa nira isiyosawazika?

Njia moja ni iwapo Mkristo angeamua kufunga ndoa na mtu asiyeamini. Kifungo hicho kingefanya hali ziwe ngumu kwa wote wawili, nao hawangekubaliana katika mambo muhimu.

Yehova alipoanzisha ndoa, alimpa mke daraka la kuwa “msaidizi.” (Mwanzo 2:18) Vivyo hivyo, kupitia nabii Malaki, Mungu alimtaja mke kuwa ‘mwenzi.’ (Malaki 2:14) Muumba wetu anataka watu waliofunga ndoa washirikiane katika mambo ya kiroho, wasaidiane na kunufaika pamoja.

Mkristo anapofunga ndoa “katika Bwana tu” anaonyesha kwamba anaheshimu shauri la Baba yetu wa mbinguni. (1 Wakorintho 7:39) Jambo hilo hufanya wenzi wa ndoa wawe na umoja, ambao unaweza kumletea Mungu sifa na heshima wakati mume na mke wanapomtumikia wakiwa ‘wenzi wa nira halisi’ katika njia ya pekee.—Wafilipi 4:3.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]

Camel and ox: From the book La Tierra Santa, Volume 1, 1830

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki