Siku ya Kukumbukwa
JIONI iliyotangulia kifo chake, Yesu Kristo alipitisha mkate usiotiwa chachu na kikombe cha divai nyekundu kwa mitume wake na kuwaagiza wale na kunywa. Pia aliwaambia hivi: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19.
Mwaka huu tukio hilo litaadhimishwa Jumapili, Aprili 4, baada ya jua kutua. Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote watakutanika jioni hiyo ili kuadhimisha Ukumbusho huo kulingana na maagizo ya Yesu. Unakaribishwa kwa uchangamfu kujiunga nao. Tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova wa eneo lenu kuhusu wakati na mahali hususa ambapo mkutano huo wa pekee utafanyiwa.