Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w04 4/1 uku. 32
  • Je, Tunapaswa Kusali kwa Malaika Watusaidie?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Tunapaswa Kusali kwa Malaika Watusaidie?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
w04 4/1 uku. 32

Je, Tunapaswa Kusali kwa Malaika Watusaidie?

JE, INAFAA kusali kwa malaika wakati wa taabu? Watu wengi hufikiri hivyo. Hata kichapo New Catholic Encyclopedia kinasema: ‘Mtu husali kwa malaika, lakini katika maana ya kwamba malaika hao waweze kutuombea kwa Mungu.’ Je, tunapaswa kusali kwa malaika ili watuombee?

Neno la Mungu hutaja majina mawili tu kati ya malaika wa Mungu waaminifu, Mikaeli na Gabrieli. (Danieli 8:16; 12:1; Luka 1:26; Yuda 9) Kwa kuwa majina hayo yanatajwa katika Biblia, tunatambua kwamba kila malaika ni kiumbe wa roho aliye na jina, wala si nguvu fulani tu isiyo na utu. Hata hivyo, malaika wengine walikataa kufunua majina yao. Kwa mfano, Yakobo alipomuuliza malaika aliyemtembelea amfunulie jina lake, malaika huyo alikataa. (Mwanzo 32:29; Waamuzi 13:17, 18) Biblia haina orodha yoyote ya majina ya malaika, na jambo hilo huwazuia wanadamu wasiwakazie malaika fikira kupita kiasi.

Mojawapo ya kazi za malaika ni kuwapitishia wanadamu ujumbe kutoka kwa Mungu. Kwa kweli, maana halisi ya maneno ya awali ya Kiebrania na Kigiriki yaliyotafsiriwa “malaika,” ni “mjumbe.” Hata hivyo, malaika si wapatanishi ambao hupeleka sala za wanadamu kwenye kiti cha enzi cha Aliye Juu Zaidi. Mungu ameamua kwamba sala zielekezwe kwake kupitia jina la Mwana wake, Yesu Kristo, aliyesema: ‘Hata mkimwomba Baba jambo gani katika jina langu, atawapa hilo.’—Yohana 15:16; 1 Timotheo 2:5.

Yehova Mungu hawi kamwe na shughuli nyingi asiweze kutusikiliza tukizungumza naye kwa njia inayofaa. Biblia hutoa uhakikisho huu: “Yehova yuko karibu na wote wanaomwitia, wote wanaomwitia yeye katika ukweli.”—Zaburi 145:18.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki