Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w04 8/15 uku. 32
  • “Hilo Ndilo Jambo Bora Zaidi Uwezalo Kufanya”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Hilo Ndilo Jambo Bora Zaidi Uwezalo Kufanya”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
w04 8/15 uku. 32

“Hilo Ndilo Jambo Bora Zaidi Uwezalo Kufanya”

ALEXIS ni mvulana mwenye umri wa miaka mitano anayeishi katika jiji la Morelia, Mexico. Wazazi wake wanajifunza Biblia na huhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova. Kwenye kusanyiko la mzunguko alilokuwa amehudhuria pamoja na wazazi wake, Alexis aliona wonyesho fulani kuhusu kuhubiri nyumba kwa nyumba. Ndipo akamgeukia babake na kumuuliza, “Baba, Baba, kwa nini huendi kuhubiri?” Babake akamjibu, “Bado ninajifunza ili niweze kuhubiri.” Kwa shauku, Alexis aliitikia, “Baba, hilo ndilo jambo bora zaidi uwezalo kufanya.”

Mtoto huyo mdogo aliona uhitaji wa kutenda kupatana na ujuzi wake kumhusu Yehova. Kwa kuwa anaishi nyumba moja na baadhi ya binamu zake wachanga, alisali kwa Yehova kwanza, kisha akazungumza nao kuhusu mambo aliyokuwa amejifunza na wazazi wake katika Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Ingawa bado Alexis hakujua kusoma, alifahamu vizuri yaliyomo katika kitabu hicho kutokana na picha zinazoandamana na masimulizi yake. Hata alisema kwamba angependa kuwatembelea watu nyumbani kwao ili kuwaeleza mambo aliyokuwa akijifunza kuhusu makusudi ya Mungu.

Kwa kweli, vijana kwa wazee wanaweza kuishi jinsi Yehova, aliye “Mtakatifu,” anavyowatarajia waishi, na hivyo kuwa na pendeleo kuu la kufanya kazi iliyo bora zaidi, kazi ya kutoa ushahidi kumhusu katika mataifa. (Isaya 43:3; Mathayo 21:16) Bila shaka, hilo ndilo jambo bora zaidi uwezalo kufanya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki