Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w04 12/1 uku. 32
  • Yale Tunayopaswa Kusoma—Shauri la Hekima la Sulemani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yale Tunayopaswa Kusoma—Shauri la Hekima la Sulemani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
w04 12/1 uku. 32

Yale Tunayopaswa Kusoma—Shauri la Hekima la Sulemani

“HAKUNA mwisho wa kutungwa kwa vitabu vingi, na kushughulika navyo sana huuchosha mwili.” (Mhubiri 12:12) Alipoandika maneno hayo miaka 3,000 hivi iliyopita, Mfalme Sulemani wa Israeli mwenye hekima hakuwa akiwazuia watu kusoma. Badala yake, alikuwa akizungumzia umuhimu wa kuwa mteuzi. Kikumbusho hicho kinafaa sana leo kwa kuwa, kila mwaka, mabilioni ya vitabu huchapishwa ulimwenguni pote!

Ni wazi kwamba “vitabu vingi” ambavyo Sulemani alitaja havikujenga wala kuburudisha. Kwa sababu hiyo alisema kwamba kujishughulisha navyo hakumletei msomaji faida za kudumu, badala yake, “huuchosha mwili.”

Hata hivyo, je, Sulemani alikuwa akisema kwamba hakuna vitabu vinavyoweza kutoa mwongozo unaofaa na wenye kutegemeka ambao unaweza kumfaidi msomaji? La, kwa kuwa aliandika hivi pia: “Maneno ya wenye hekima ni kama michokoo ya kuongoza ng’ombe, na kama tu misumari iliyopigiliwa ndani, ndivyo walivyo wale wanaoshughulika mno kukusanya maneno; wametolewa kutoka kwa mchungaji mmoja.” (Mhubiri 12:11) Kwa kweli, kuna maneno yaliyoandikwa ambayo, “kama michokoo” yanaweza kuchochea ifaavyo. Yanaweza kumchochea mtu afuate njia inayofaa. Isitoshe, ‘kama misumari iliyopigiliwa ndani,’ maneno hayo yanaweza kuimarisha na kutia nguvu azimio la mtu.

Tunaweza kupata wapi maneno hayo ya hekima? Kulingana na Sulemani, maneno muhimu zaidi ni yale yanayotoka kwa Mchungaji mmoja Yehova. (Zaburi 23:1) Kwa hiyo, mtu anaweza kupata maneno hayo ya hekima kutoka katika kitabu bora zaidi kilichoandikwa na roho ya Mungu, yaani, Biblia. Kusoma kwa ukawaida maneno hayo yaliyoongozwa na roho kunaweza kumsaidia mtu “awe na uwezo kamili, akiwa na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.”—2 Timotheo 3:16, 17.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki