Mwaliko . . .
Je, Bado Mungu Ana Mamlaka Juu ya Dunia?
MISIBA ya asili, magonjwa hatari, ufisadi miongoni mwa watu wenye mamlaka, mashambulizi ya kigaidi, vita, na uhalifu. Karibu kila siku tunasikia habari kama hizo. Uwe umeathiriwa na mambo hayo au la, sisi hutaka kujua ulimwengu huu unaelekea wapi na ikiwa hali itakuwa bora wakati ujao.
Mambo hayo yatazungumziwa katika hotuba ya watu wote itakayotolewa na Mashahidi wa Yehova katika nchi zaidi ya 200 ulimwenguni. Kichwa cha hotuba hiyo kitakuwa: “Je, Bado Mungu Ana Mamlaka Juu ya Dunia?” Hotuba hiyo ya wakati unaofaa itazungumzia yale ambayo Mungu anasema na kuahidi katika Neno lake lenye kutegemeka, Biblia. Itajibu maswali haya muhimu:
Je, Mungu anapendezwa na mambo yanayotendeka duniani?
Anawaonaje wanadamu?
Je, anakujali?
Katika sehemu nyingi, hotuba hiyo itatolewa Jumapili, Aprili 30, 2006, katika Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova. Mashahidi katika eneo lenu watafurahi kukujulisha mahali na wakati ambapo hotuba hiyo itatolewa.
Unaalikwa kwa uchangamfu uhudhurie hotuba hiyo yenye kutia moyo inayotegemea Biblia, nawe hutatozwa chochote. Hotuba hiyo itakupa jibu lenye kuridhisha kwa swali hili: Je, Bado Mungu Ana Mamlaka Juu ya Dunia?