Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w06 10/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Habari Zinazolingana
  • Musa—Jinsi Maisha Yake Yanavyokuhusu
    Amkeni!—2004
  • Kitabu Cha Biblia Namba 5—Kumbukumbu La Torati
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Yesu Kristo Alikuwaje Nabii Kama Musa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
w06 10/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Kwa nini katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya andiko la Kumbukumbu la Torati 31:2 linasema kwamba Musa ‘hangeruhusiwa tena kutoka nje na kuingia ndani’ akiwa kiongozi wa Israeli, huku tafsiri nyingine zikionyesha kwamba hangeweza tena kufanya hivyo?

Ingawa neno la Kiebrania linalozungumziwa hapo linaweza kutafsiriwa kwa njia zote mbili, tafsiri fulani za Kiswahili za Biblia zinaonyesha kwamba karibu na mwisho wa maisha yake, Musa alikuwa dhaifu kimwili, na hangeweza kutimiza madaraka yake akiwa kiongozi. Kwa mfano, tafsiri ya Union Version inamnukuu Musa akisema hivi: “Mimi leo ni mwenye miaka mia na ishirini; siwezi tena kutoka na kuingia.” Vivyo hivyo, Biblia Habari Njema inasema hivi: “Sina nguvu ya kufanya kazi zaidi.”

Hata hivyo, andiko la Kumbukumbu la Torati 34:7 linaonyesha kwamba hata ingawa Musa alikuwa na umri mkubwa, hakuwa dhaifu kimwili. Andiko hilo linasema hivi: “Musa alikuwa na umri wa miaka 120 wakati wa kifo chake. Jicho lake halikuwa limeingia giza, na nguvu zake hazikuwa zimepotea.” Hivyo, Musa alikuwa na nguvu za kuongoza taifa hilo, lakini Yehova hakutaka aendelee kufanya hivyo. Hilo linaonyeshwa na maneno haya ya Musa: “Kama vile Yehova alivyoniambia, ‘Wewe hutavuka mto huu wa Yordani.’” Yaonekana Yehova alikuwa anarudia yale aliyosema kwenye maji ya Meriba.—Hesabu 20:9-12.

Musa aliishi maisha marefu na ya pekee, ambayo yanaweza kugawanywa katika sehemu tatu. Kwa miaka 40 alikaa Misri, ambako ‘alifundishwa hekima yote ya Wamisri’ na alikuwa “mwenye nguvu katika maneno na matendo.” (Matendo 7:20-22) Kwa miaka mingine 40, aliishi Midiani. Akiwa huko, alisitawisha sifa za kiroho zilizohitajiwa ili kuwaongoza watu wa Yehova. Mwishowe, Musa aliwaongoza na kuwasimamia Waisraeli kwa miaka 40. Hata hivyo, sasa Yehova aliamua kwamba Yoshua, bali si Musa, ndiye angeliongoza taifa hilo kuvuka Mto Yordani na kuingia Nchi ya Ahadi.—Kumbukumbu la Torati 31:3.

Hivyo, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inaonyesha kwa usahihi maana ya andiko la Kumbukumbu la Torati 31:2. Musa hangeendelea kuwa kiongozi wa Israeli, si kwa sababu hakuwa na uwezo wa kimwili, bali kwa sababu Yehova hakumruhusu afanye hivyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki