Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 6/15 uku. 32
  • “Je, Unajua Jina la Mungu?”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Je, Unajua Jina la Mungu?”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 6/15 uku. 32

“Je, Unajua Jina la Mungu?”

SWALI hilo liliamsha upendezi wa mwanamke fulani huko kusini-magharibi mwa Asia ya Kati. Swali hilo lilikuwa katika jalada la toleo la Januari 22, 2004 (22/1/2004), la gazeti letu la Amkeni! Mwanamke huyo aliwaandikia hivi wachapishaji wa gazeti hilo: “Tangu mwanzo nilivutiwa kusoma kwa ukawaida gazeti lenu la Amkeni!, nalo lilinisaidia kupendezwa na viwango bora vya maadili. Maoni yangu kuhusu uhai yanazidi kuwa mazuri. Ninamwambia kila mtu kuhusu Mungu wetu na amani inayoletwa na ujuzi huo.”

Katika maeneo mengi, ndiyo, “mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia,” watu wanajulishwa jina la Mungu, Yehova. (Matendo 1:8) Kwa mfano, Yehowa, ambalo ndilo jina la Mungu katika lugha ya Turkmen, linapatikana mara nyingi katika tafsiri ya Turkmen ya Maandiko Matakatifu. Zaburi 8:1 inasema: “Yehova Bwana wetu, jina lako ni lenye utukufu kama nini katika dunia yote!”

Ili ajifunze mengi zaidi kumhusu Yehova Mungu, mwanamke huyo aliomba broshua yenye kurasa 32 iliyo na kichwa Jina la Mungu Litakaloendelea Milele. Wewe pia unaweza kuwaomba Mashahidi wa Yehova wakuletee broshua hiyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki