Masomo Muhimu kwa Vijana
GLADYS anafanya kazi katika shule moja huko Mendoza, Argentina. Siku moja alipita katika darasa moja naye akaona mwalimu mmoja wa kike akiwasomea wanafunzi wake wenye umri wa kati ya miaka 9 na 10 Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.a Gladys alijitambulisha kwa mwalimu huyo kuwa Shahidi wa Yehova na akamwambia kwamba angependa kumwonyesha jinsi ya kufaidika zaidi na kichapo hicho. Kwa kuwa alivutiwa na yale ambayo Gladys alimwambia, mwalimu huyo alitaka kitabu hicho kitumiwe kwa ukawaida kikiwa sehemu ya masomo. Hata hivyo, mwalimu huyo alihitaji kwanza kupewa ruhusa na wakuu wa shule. Alifurahi sana aliporuhusiwa kufanya hivyo.
Baadaye, wakati wa programu ya Siku ya Kusoma Vitabu, mwalimu huyo aliwapa wanafunzi wake mgawo wa kusoma sura moja ya kitabu hicho mbele ya wanafunzi wenzao. Kwa sababu ya matokeo mazuri ya programu hiyo, mwalimu huyo alialikwa kuwa mgeni katika kipindi cha televisheni ya mahali hapo. Wakati mwenendo wa wanafunzi ulipotajwa, mtayarishaji wa kipindi hicho alimuuliza hivi mwalimu huyo, “Unafanya nini ili watoto wajiendeshe vizuri darasani?” Mwalimu huyo alieleza kwamba anatumia kichapo kinachoitwa Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia. Alieleza kwamba hafundishi dini katika darasa lake, hata hivyo kupitia kitabu hicho, anawafundisha wanafunzi wake sifa bora za maadili au mwenendo mwema kama vile heshima, kuvumiliana, umoja, ushirikiano, utii, na upendo. Wote walikubali kwamba vijana wanahitaji kujifunza mambo hayo muhimu.
Je, ungependa kufundisha watoto wako sifa za maadili kama hizo? Unaweza kumwomba mmoja wa Mashahidi wa Yehova nakala ya kichapo hiki chenye kuvutia sana, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.
[Maelezo ya Chini]
a Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.