Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 4/1 kur. 7-8
  • Kuzaliwa Upya—Kusudi Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzaliwa Upya—Kusudi Ni Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni, na kwa Sababu Gani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Wachache Watawala, Wengi Wanufaika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Serikali ltakayoleta Amani Duniani Pote
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 4/1 kur. 7-8

Kuzaliwa Upya—Kusudi Ni Nini?

WATU wengi wanaamini kwamba mtu anahitaji kuzaliwa tena ili kupokea wokovu wa milele. Hata hivyo, ona vile Yesu mwenyewe alivyosema kuhusu kusudi la kuzaliwa upya. Alisema: “Mtu asipozaliwa tena, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.” (Yohana 3:3) Hivyo, mtu anahitaji kuzaliwa tena ili kuingia katika Ufalme wa Mungu, si ili kupata wokovu. Huenda wengine wakauliza, ‘Je, semi hizi mbili—kuingia katika Ufalme, na kupata wokovu—zinarejelea thawabu ileile?’ Hapana. Ili kuelewa tofauti, tutafikiria kwanza maana ya maneno “ufalme wa Mungu.”

Ufalme ni aina fulani ya serikali. Kwa hiyo, maneno “ufalme wa Mungu” yanamaanisha “serikali ya Mungu.” Biblia inafundisha kwamba Yesu Kristo, “mwana wa binadamu,” ndiye Mfalme wa Ufalme wa Mungu na kwamba Kristo atatawala pamoja na wengine. (Danieli 7:1, 13, 14; Mathayo 26:63, 64) Isitoshe, maono fulani ambayo mtume Yohana alipokea yanafunua kwamba wale watakaotawala pamoja na Kristo wamechaguliwa “kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa,” nao “watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Ufunuo 5:9, 10; 20:6) Pia, Neno la Mungu linafunua kuwa wale watakaotawala wakiwa wafalme ni “kundi dogo” la watu 144,000 “ambao wamenunuliwa kutoka duniani.”—Luka 12:32; Ufunuo 14:1, 3.

Ufalme wa Mungu uko wapi? “Ufalme wa Mungu” pia unaitwa “ufalme wa mbinguni,” jambo linaloonyesha kwamba Yesu na wafalme wenzake watatawala kutoka mbinguni. (Luka 8:10; Mathayo 13:11) Hivyo, Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni ambayo mtawala wake ni Yesu Kristo pamoja na kikundi cha watawala wenzake ambao wamechaguliwa kutoka kati ya wanadamu.

Kwa hiyo, Yesu alimaanisha nini aliposema ni lazima mtu azaliwe tena ili “kuingia katika ufalme wa Mungu”? Alimaanisha kwamba mtu anahitaji kuzaliwa tena ili awe mtawala pamoja na Kristo mbinguni. Kwa wazi, kusudi la kuzaliwa upya ni kutayarisha kikundi cha wanadamu wachache kuwa watawala mbinguni.

Kufikia hapa, tumeona kwamba kuzaliwa upya ni muhimu sana, Mungu ndiye anayeamua kama mtu atazaliwa upya, na kwamba kuzaliwa upya kunawatayarisha wanadamu fulani kuwa watawala mbinguni. Lakini mtu anazaliwa upya jinsi gani?

[Blabu katika ukurasa wa 7]

Kusudi la kuzaliwa upya ni kutayarisha kikundi cha wanadamu wachache kuwa watawala mbinguni

[Picha katika ukurasa wa 7]

Yesu Kristo na kikundi cha wanadamu waliochaguliwa kutoka kati ya wanadamu watatawala katika Ufalme wa Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki