Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 1/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Jina la Mungu
    Amkeni!—2017
  • Kwa Nini Tunapaswa Kutumia Jina la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Je, Mungu Ana Jina?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Unalijua na Kulitumia Jina la Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/1 uku. 16

Majibu ya Maswali ya Biblia

Jina la Mungu ni nani?

Watu wote katika familia zetu wana majina ya kibinafsi. Hata wanyama wa kufugwa wana majina! Je, si jambo linalopatana na akili kwa Mungu kuwa na jina? Katika Biblia, Mungu ana majina mengi ya cheo, kama vile, Mungu Mweza-Yote, Bwana Mwenye Enzi Kuu, na Muumba, lakini pia ana jina la kibinafsi.—Soma Isaya 42:8.

Tafsiri nyingi za Biblia zina jina la kibinafsi la Mungu kwenye Zaburi 83:18. Kwa mfano, kwenye Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, andiko hilo linasema: “Ili watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova, wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.”

Kwa nini tunapaswa kulitumia jina la Mungu?

[Picha katika ukurasa wa 16]

Tunatumia majina ya kibinafsi tunapozungumza na watu tunaowapenda, kama vile rafiki zetu wa karibu

Mungu anataka tulitumie jina lake la kibinafsi. Tunatumia majina ya kibinafsi tunapozungumza na watu tunaowapenda, kama vile rafiki zetu wa karibu, hasa wanapotuomba tutumie majina yao. Je, haipaswi kuwa hivyo pia tunapozungumza na Mungu? Zaidi ya hayo, Yesu Kristo aliwatia moyo watu watumie jina la Mungu.—Soma Mathayo 6:9; Yohana 17:26.

Hata hivyo, ili tuwe rafiki za Mungu, tunapaswa kujua mengi zaidi kumhusu mbali tu na kujua jina lake. Kwa mfano, Mungu ana mwili wa aina gani? Je, kweli inawezekana kumkaribia Mungu? Unaweza kupata majibu ya maswali hayo katika Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki