Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 11/1 uku. 16
  • Ni Nani Watakaoenda Mbinguni​—Je, Ni Watu Wote Wazuri?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Watakaoenda Mbinguni​—Je, Ni Watu Wote Wazuri?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Wanaoenda Mbinguni, na kwa Sababu Gani?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Je, Wakristo Wote Waaminifu Wanaenda Mbinguni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Je, Watu Wote Wazuri Wanaenda Mbinguni?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 11/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Ni nani watakaoenda mbinguni na kwa nini?

Mamilioni ya watu wanatazamia kwenda mbinguni watakapokufa. Yesu alisema kwamba mitume wake waaminifu ndio watakaoishi mbinguni. Kabla ya kufa, aliahidi kuwatayarishia mahali ili waishi na Baba yake aliye mbinguni.​—Soma Yohana 14:2.

Kwa nini watu walio duniani watafufuliwa na kwenda kuishi mbinguni? Watafanya nini huko? Yesu aliwaambia mitume wake kwamba watakuwa wafalme. Wataitawala dunia.​—Soma Luka 22:28-30; Ufunuo 5:10.

Je, watu wote wazuri huenda mbinguni?

Katika nchi nyingi, watu wachache tu ndio hutawala. Kwa kuwa Yesu anawafufua watu fulani wakaishi mbinguni ili watawale dunia, tunaweza kutazamia kwamba wachaguliwa hao ni wachache. (Luka 12:32) Biblia inataja idadi ya watu watakaotawala pamoja na Yesu.​—Soma Ufunuo 14:1.

Yesu amewatayarishia baadhi ya wafuasi wake makao mbinguni. Je, unajua watafanya kazi gani huko?

Mbali na wale wanaoenda mbinguni, watu wengine pia watathawabishwa. Raia waaminifu wa Ufalme wa Yesu watafurahia kuishi milele katika dunia itakayokuwa paradiso. (Yohana 3:16) Wengine wataingia katika Paradiso baada ya kuokoka uharibifu wa mfumo huu mwovu wa mambo na wengine wataingia baada ya kufufuliwa.​—Soma Zaburi 37:29; Yohana 5:28, 29.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kukipakua kwenye

www.jw.org

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki