Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 8/1 uku. 4
  • Mungu Anakutazama

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Anakutazama
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Sikiliza, Jifunze, na Uonyeshe Huruma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • “Tukio la Mfano” Ambalo Ni Muhimu Kwetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Tafuta Mwongozo wa Mungu Katika Kila Jambo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 8/1 uku. 4

HABARI KUU? | JE, MUNGU ANAKUJALI?

Mungu Anakutazama

“Kwa maana macho yake [Mungu] yako juu ya njia za mwanadamu, Naye huziona hatua zake zote.”—AYUBU 34:21.

Baba akicheza na mvulana wake

Mtoto mdogo zaidi ya wote ndiye anayehitaji kutunzwa sana

KWA NINI WENGINE HAWAAMINI? Kulingana na utafiti wa hivi karibuni, galaksi yetu peke yake ina sayari bilioni 100 hivi. Kwa sababu ya ukubwa wa ulimwengu wote, watu wengi hujiuliza, ‘Kwa nini Muumba atazame wanadamu duni kwenye sayari ndogo sana?’

BIBLIA INAFUNDISHA NINI? Mungu hakutupatia Biblia kisha akatuacha. Badala yake, Yehova anatuhakikishia hivi: “Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.”—Zaburi 32:8.

Mfikirie Hagari, mwanamke Mmisri aliyeishi karne ya 20 K.W.K. Hagari alishindwa kumheshimu mwajiri wake, Sarai, kwa hiyo akafedheheshwa na akakimbilia nyikani. Kwa sababu Hagari alikuwa amefanya kosa, je, Mungu aliacha kumjali? Biblia inasema hivi: “Malaika wa Yehova akamkuta.” Malaika huyo alimhakikishia hivi Hagari: “Yehova ameyasikia mateso yako.” Kisha Hagari akamwambia Yehova hivi: “Wewe ni Mungu mwenye kuona.”—Mwanzo 16:4-13.

“Mungu mwenye kuona” anakutazama wewe pia. Kwa mfano: Mama mwenye upendo huwatazama kwa makini watoto wake wadogo, kwa sababu mtoto mdogo zaidi ya wote ndiye anayehitaji kutunzwa sana. Vivyo hivyo, Mungu hututazama hasa tunapokuwa dhaifu na tunapokabili hatari. Yehova anasema hivi: “Mimi ninakaa kileleni na katika mahali patakatifu, pia pamoja na mtu aliyepondwa na mwenye roho ya unyenyekevu, ili kuipa uhai roho ya watu wa hali ya chini na kuupa uhai moyo wa wale wanaopondwa.”—Isaya 57:15.

Hata hivyo, huenda ukajiuliza: ‘Mungu ananitazama jinsi gani? Je, yeye hunihukumu kwa kuangalia tu sura yangu, au huchunguza moyo wangu?’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki