Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 8/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Unawezaje Kuitambua Ibada ya Kweli?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Kuna Habari Gani Kuhusu Dini?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Unaweza Kuitambua Ibada ya Kweli Jinsi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ibada Ambayo Mungu Anakubali
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 8/1 uku. 16
Mashahidi wa Yehova kutoka jamii mbalimbali wakiwa katika Jumba la Ufalme

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Je, dini zote zinampendeza Mungu?

Unaposikiliza taarifa za habari, huenda umesikia kwamba nyakati nyingine mambo mabaya hufanywa kwa sababu za kidini. Si dini zote zinazompendeza Mungu. (Mathayo 7:15) Kwa kweli, wanadamu wengi wamepotoshwa.—Soma 1 Yohana 5:19.

Hata hivyo, Mungu anawajua watu wanyoofu wanaopenda mambo yaliyo mema na ya kweli. (Yohana 4:23) Mungu anawaalika watu kama hao wajifunze ukweli wa Neno lake, Biblia.—Soma 1 Timotheo 2:3-5.

Unawezaje kuitambua dini ya kweli?

Yehova Mungu anawaunganisha watu ambao wametoka katika dini mbalimbali kwa kuwafundisha ukweli na kupendana pia. (Mika 4:2, 3) Hivyo, unaweza kuwatambua wafuasi wa dini ya kweli kutokana na vile wanavyopendana.—Soma Yohana 13:35.

Yehova Mungu anawaunganisha watu wa namna zote katika ibada ya kweli.—Zaburi 133:1

Biblia ndiyo msingi wa imani na maisha ya wafuasi wa dini ya kweli. (2 Timotheo 3:16) Wanaliheshimu pia jina la Mungu. (Zaburi 83:18) Wanatangaza kwamba Ufalme wa Mungu ndilo tumaini pekee kwa ajili ya wanadamu. (Danieli 2:44) Wanamwiga Yesu kwa kuacha ‘nuru yao iangaze,’ na kuwatendea jirani zao mema. (Mathayo 5:16) Hivyo, Wakristo wa kweli, wanaweza kutambuliwa kwa vile wanawatembelea watu nyumbani ili wazungumze nao kuhusu habari njema za Ufalme wa Mungu.—Soma Mathayo 24:14; Matendo 5:42; 20:20.

Kwa habari zaidi soma sura ya 15 ya kitabu hiki kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Kinapatikana pia kwenye www.jw.org/sw

SOMA MAJIBU YA MASWALI ZAIDI YA BIBLIA KWENYE INTANETI

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki