Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 9/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Malaika Ni Nani?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Viumbe wa Roho Wanahusikaje Katika Maisha Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Malaika—Jinsi Wanavyohusika Katika Maisha Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Malaika—“Roho kwa Ajili ya Utumishi wa Watu Wote”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 9/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Je, malaika wanaweza kutusaidia?

Danieli akiwa ndani ya shimo la simba akiwa amelindwa na malaika

Kama walivyomsaidia Danieli mtumishi mwaminifu wa Mungu, leo malaika huwasaidia watu kusikia habari njema

Yehova Mungu aliumba mamilioni ya malaika muda mrefu kabla ya kuwaumba wanadamu. (Ayubu 38:4, 7) Malaika hao ni viumbe wa roho wenye nguvu ambao wanamtumikia Mungu, na nyakati nyingine yeye huwatuma kuwaongoza na kuwalinda watumishi wake duniani. (Zaburi 91:10, 11) Leo, malaika wanawasaidia watu kusikia habari njema inayohubiriwa na wafuasi wa Yesu.—Soma Ufunuo 14:6, 7.

Je, tunapaswa kusali kwa malaika ili watusaidie? Hapana. Sala inahusiana na ibada, na Mungu peke yake ndiye anayepaswa kuabudiwa. (Ufunuo 19:10) Malaika ni watumishi wa Mungu, kwa hiyo wao husikiliza maagizo yake bali si ya wanadamu. Hivyo, tunapaswa kusali sikuzote kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.—Soma Zaburi 103:20, 21; Mathayo 26:53.

Je, kuna malaika wabaya?

Kama wanadamu, malaika waliumbwa wakiwa na uhuru wa kuchagua kutenda mema au mabaya. Kwa kusikitisha, malaika wengi walimwasi Mungu. (2 Petro 2:4) Shetani ndiye aliyekuwa wa kwanza kuasi; kisha wengine wakamfuata na kuwa roho waovu. Hivi karibuni, Shetani na roho waovu walifukuzwa kutoka mbinguni na kutupwa duniani.—Soma Ufunuo 12:7-9.

Ongezeko kubwa la uovu na jeuri tangu mwaka wa 1914 ni ishara kwamba hivi karibuni Mungu atamkomesha Shetani na roho waovu. Kisha Mungu atarudisha hali bora kabisa duniani.—Soma Ufunuo 12:12; 21:3, 4.

Kwa habari zaidi soma sura ya 10 ya kitabu hiki kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia, kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki