Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 10/1 kur. 8-9
  • Ufalme wa Mungu​—Utakuwa na Umuhimu Gani Kwako?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufalme wa Mungu​—Utakuwa na Umuhimu Gani Kwako?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Ufalme wa Mungu​—Una Umuhimu Gani kwa Yesu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Ufalme Wa Mungu
    Amkeni!—2013
  • Amua Kuunga Mkono Ufalme wa Mungu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2020
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 10/1 kur. 8-9
Mume na mke wakifundishwa kuhusu Ufalme wa Mungu

HABARI KUU | UFALME WA MUNGU—UNA UMUHIMU GANI KWAKO?

Ufalme wa Mungu​— Utakuwa na Umuhimu Gani Kwako?

Huenda katika makala zilizotangulia umejifunza kwamba Mashahidi wa Yehova wanathamini sana Ufalme wa Mungu. Na labda umevutiwa na baadhi ya baraka za wakati ujao za Ufalme wa Mungu zilizozungumziwa katika makala hizo. Na wakati huohuo huenda umejiuliza ikiwa kweli ahadi hizo zitatimia.

Ni jambo la hekima kuwa na tahadhari badala ya kuamini kila neno unalosikia. (Methali 14:15) Kwa njia fulani, mtazamo huo unalingana na ule wa Waberoya wa kale.a Waliposikia habari njema za Ufalme kwa mara ya kwanza, Waberoya walikubali waliyoyasikia, lakini si kwa sababu tu walitaka yawe ya kweli. Badala yake, walichunguza Maandiko kwa uangalifu “ili kuona kama mambo hayo ndivyo yalivyo.” (Matendo 17:11) Kwa maneno mengine, Waberoya walilinganisha Maandiko na habari njema walizosikia. Baada ya muda walisadiki kwamba habari njema zilitegemea kabisa Neno la Mungu.

Mashahidi wa Yehova wanakuomba ufanye hivyo pia. Kupitia mpango wetu wa kujifunza Biblia bila malipo, utapata nafasi ya kulinganisha yale ambayo Mashahidi wa Yehova wanaamini kuhusu Ufalme wa Mungu na yale ambayo Biblia inafundisha.

Zaidi ya kujifunza kuhusu Ufalme wa Mungu, kujifunza Biblia kutakusaidia kupata majibu ya maswali muhimu maishani.

  • Tulitoka wapi?

  • Ni nini kusudi la maisha?

  • Kwa nini Mungu anaruhusu watu wateseke?

  • Ni nini hutupata tunapokufa?

  • Je, dunia itaharibiwa?

  • Ni nini siri ya kuwa na familia yenye furaha?

Jambo muhimu zaidi, kujifunza Biblia kutakusaidia ‘kumkaribia Mungu.’ (Yakobo 4:8) Kadiri unavyozidi kumkaribia Mungu ndivyo utakavyoona jinsi Ufalme wa Mungu ulivyo muhimu kwako—si wakati huu tu, bali pia milele. Yesu mwenyewe alisali hivi: “Uzima wa milele ndio huu, waendelee kupata ujuzi juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.”—Yohana 17:3.

Mashahidi wa Yehova wanaweza kutumia kitabu hiki kujifunza Biblia pamoja nawe.

Ili kujifunza Biblia bila malipo, waombe Mashahidi wa Yehova au ujaze fomu inayopatikana kwenye tovuti ya www.jw.org/sw. (Bofya OMBA UFUNDISHWE BIBLIA kwenye ukurasa wa kwanza)

a Beroya lilikuwa jiji la Makedonia ya kale.

Umuhimu wa Ufalme wa Mungu kwa Msichana Mdogo

Folake

Hivi karibuni, Folake msichana mwenye umri wa miaka 10 aliombwa aandike insha shuleni yenye kichwa “Ninachopenda Zaidi Ulimwenguni.” Folake alichagua kuandika kuhusu jinsi anavyofurahia kuzungumza na wengine kuhusu Ufalme wa Mungu.

Folake aliandika hivi: “Ufalme wa Mungu ni serikali halisi. Lakini huwezi kuiona—hata ukivaa miwani!”

Kisha Folake akaandika kuhusu baraka za Ufalme huo ambazo anazitarajia. Alitaja baadhi ya matatizo ambayo Ufalme huo utatatua, alipoandika: “Ninahuzunika ninapoona watu wasio na makao wakiishi barabarani” pia “watoto wakifa kwa kukosa chakula katika sehemu mbalimbali ulimwenguni.” Aliongeza hivi: “Ninapata furaha ninaposoma Isaya 65:21.” Kuhusu wanadamu watakaoishi chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu, mstari huo unasema hivi: “Watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.”

Folake aliandika kwamba anangoja kwa hamu wakati ambapo Mungu, kwa kutumia Ufalme wake, ataondoa magonjwa yote. Katika insha yake, alinukuu andiko la Ufunuo 21:4, linalosema kwamba Mungu “atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” Alimalizia kwa kusema tena kwamba anachopenda zaidi ulimwenguni ni kuzungumza kuhusu Yehova na Ufalme wake. Bila shaka, msichana huyu anapenda sana Ufalme wa Mungu!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki