Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 11/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari Zinazolingana
  • Kutakuwa na Ufufuo!
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Wapendwa Wako Wanaweza Kuwa Hai Tena!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ufufuo—wa Nani, na Wapi?
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 11/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Je, kweli Yesu aliwafufua wafu?

Yesu alimfufua Lazaro kwa kumwita kutoka kaburini

Yesu alimfufua Lazaro aliyekuwa amekufa kwa siku nne

Biblia inasema waziwazi kwamba Yesu aliwafufua watu waliokufa. Masimulizi hayo si hadithi tu, kwani yalifanyika wakati na mahali hususa. Kwa mfano, katika majira ya kiangazi ya mwaka wa 31 W.K., umati mkubwa ulisafiri pamoja na Yesu kutoka Kapernaumu hadi Naini. Walipofika walikutana na umati mwingine. Punde baada ya hapo kijana aliyekufa alifufuliwa na tunaweza kuamini kwa sababu ufufuo huo umesimuliwa katika Neno la Mungu, Biblia, na ulishuhudiwa na watu hao wote.—Soma Luka 7:11-15.

Yesu, pia alimfufua rafiki yake Lazaro aliyekuwa amekufa kwa siku nne. Unaweza kuamini jambo hilo pia kwa sababu lilishuhudiwa na watu wengi.—Soma Yohana 11:39-45.

Kwa nini Yesu aliwafufua wafu?

Yesu aliwafufua wafu kwa sababu alikuwa na huruma. Vilevile, alifanya hivyo ili kuonyesha kwamba Baba yake, Muumba wa viumbe vyote, alikuwa amempa nguvu za kushinda kifo.—Soma Yohana 5:21, 28, 29.

Kwa kuwa Yesu aliwafufua wafu, tunaweza kuamini ahadi zake za wakati ujao. Atawafufua watu wengi, kutia ndani wasio waadilifu ambao hawakumjua Mungu wa kweli. Watapewa nafasi ya kumjua na kumpenda Yehova Mungu.—Soma Matendo 24:15.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 7 ya kitabu, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki