Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 2/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mungu Ataleta Serikali Itakayotawala Ulimwengu Mzima?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Serikali ya Mungu ya Amani
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 2/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Je, inawezekana ulimwengu wote kutawaliwa na serikali moja?

Watu wa mataifa yote wakiwa wameunganishwa na serikali ya ulimwenguni pote

Serikali ya ulimwenguni pote inawezaje kuwaunganisha watu wa mataifa yote? Isaya 32:1, 17; 54:13

Fikiria faida ambazo wanadamu wangepata ikiwa kungekuwa na serikali moja tu duniani pote. Leo watu wengi wanateseka kwa sababu ya umaskini ilhali wengine ni matajiri sana. Hata hivyo, serikali inayowajali watu itahakikisha kwamba kila mtu duniani anapata mahitaji yake. Je, wanadamu wanaweza kuunda serikali kama hiyo?—Soma Yeremia 10:23.

Historia inaonyesha kwamba serikali za wanadamu zimeshindwa kuwatimizia mahitaji raia na hasa maskini. Serikali nyingine zinatawala kwa ukatili. (Mhubiri 4:1; 8:9) Hata hivyo, Mungu Mweza-Yote ameahidi kwamba serikali yake itachukua mahali pa serikali za wanadamu. Mtawala wa serikali hiyo atawatimizia watu mahitaji yao yote.—Soma Isaya 11:4; Danieli 2:44.

Ufalme wa Mungu utafanya nini?

Yehova Mungu amemchagua Mtawala anayefaa kabisa kuutawala ulimwengu, yaani, Mwana wake Yesu. (Luka 1:31-33) Alipokuwa duniani, Yesu alipenda kuwasaidia watu. Akiwa Mfalme, ataleta umoja miongoni mwa watu wa mataifa yote na kuwaondolea mateso.—Soma Zaburi 72:8, 12-14.

Je, watu wote wanamkubali Yesu kuwa Mtawala? La hasha! Hata hivyo, Yehova ni mwenye subira. (2 Petro 3:9) Anawapa watu nafasi ya kumkubali Yesu kuwa Mtawala. Hivi karibuni, Yesu atawaondoa waovu na kuleta amani na usalama ulimwenguni pote.—Soma Mika 4:3, 4.

Kwa habari zaidi, soma sura ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia, kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki