Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 5/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nini Kitakachotokea Katika Siku ya Hukumu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Siku ya Hukumu na Baada ya Hapo
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Siku ya Hukumu Ni Nini?
    Amkeni!—2010
  • Siku ya Hukumu
    Ufahamu wa Kina wa Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 5/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Siku ya Hukumu ni nini?

Washiriki wa familia wakiwa na shangwe baada ya kufufuliwa wakati wa kipindi cha miaka elfu moja

Kwa nini siku ya hukumu itakuwa kipindi chenye furaha?

Katika nyakati za Biblia, Mungu alitumia waamuzi kuwaokoa watu wake kutokana na ukosefu wa haki. (Waamuzi 2:18) Biblia inasema kwamba Siku ya Hukumu inayokuja itakuwa pindi yenye furaha kwa kuwa Yehova, Mwamuzi wa dunia yote, ataondoa ukosefu wa haki unaowapata wanadamu.—Soma Zaburi 96:12, 13; Isaya 26:9.

Mungu amemweka rasmi Yesu kuwa mwamuzi wa walio hai na wafu. (Matendo 10:42; 17:31) Watu wengi wamekufa bila kupata nafasi ya kumjua Mungu. Katika Siku ya Hukumu, Yesu atawafufua watu hao ili wamjue na kumpenda Mungu wa kweli.—Soma Matendo 24:15.

Kwa nini Siku ya Hukumu itakuwa na urefu wa miaka elfu moja?

Wafu watafufuliwa wakati wa kipindi cha miaka elfu moja. (Ufunuo 20:4, 12) Watahitaji kutumia wakati ili kujifunza njia za Mungu na kumtii. Tofauti na maoni ya watu wengi, Biblia inaonyesha kwamba watu watahukumiwa kwa msingi wa matendo yao baada ya kufufuliwa.—Soma Waroma 6:7.

Biblia inataja pia kuhusu siku ya hukumu itakayotukia ghafla kabla kipindi cha miaka elfu moja kuanza. Siku hiyo huitwa pia mwisho kama ilivyotajwa katika makala za habari kuu zilizo katika toleo hili. Katika siku hiyo, Mungu atawaangamiza waovu. (2 Petro 3:7) Hivyo, tunapaswa kuonyesha wazi kwamba tunampenda Mungu.—Soma 2 Petro 3:9, 13.

Kwa habari zaidi, tazama ukurasa wa 213 wa kitabu, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia linapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki