Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 8/1 kur. 7-8
  • Tumaini kwa Wafu​—Unawezaje Kuwa na Uhakika?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tumaini kwa Wafu​—Unawezaje Kuwa na Uhakika?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini la Ufufuo Ni Hakika!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Tumaini la Ufufuo Ni Hakika!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Tumaini la Ufufuo Lina Nguvu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 8/1 kur. 7-8

HABARI KUU | UHAI BAADA YA KIFO​—JE, HILO LINAWEZEKANA?

Tumaini Kwa Wafu Unawezaje Kuwa na Uhakika?

Je, ni sahihi kuamini kwamba wafu wataishi tena? Mtume Paulo aliamini hivyo. Aliongozwa na roho takatifu kuandika hivi: “Ikiwa ni katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi ndio wa kusikitikiwa zaidi kati ya watu wote. Hata hivyo, sasa Kristo amefufuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo.” (1 Wakorintho 15:19, 20) Paulo aliona ufufuo kuwa jambo halisi. Alikuwa na uhakika huo kwa sababu Yesu mwenyewe alifufuliwa.a (Matendo 17:31) Ndiyo sababu Paulo alimwita Yesu “matunda ya kwanza” yaani, alikuwa mtu wa kwanza kufufuliwa na kupewa uzima wa milele. Ikiwa Yesu alikuwa wa kwanza, ni wazi kwamba kungekuwa na wengine ambao wangefufuliwa.

Mwanamke akisoma Biblia na kupata tumaini hakika la wakati ujao

Ayubu alimwambia hivi Mungu: “Utaitamani sana kazi ya mikono yako.”​—Ayubu 14:14, 15

Kuna sababu nyingine inayoweza kukupatia uhakika wa tumaini la ufufuo. Yehova ni Mungu wa kweli. ‘Mungu hawezi kusema uwongo.’ (Tito 1:2) Yehova hajawahi na hatawahi kamwe kusema uwongo. Je, angeahidi kuhusu ufufuo, hata kutuonyesha kwamba anaweza kufufua wafu na kisha asitende kulingana na ahadi yake? Jambo hilo halipatani na akili hata kidogo!

Kwa nini Yehova ameahidi kufufua wafu wakati ujao? Kwa sababu ya upendo. Ayubu aliuliza hivi: “Mtu akifa, je, anaweza kuishi tena?” Kisha akasema hivi: “Wewe utaita, na mimi mwenyewe nitakujibu. Kwa kuwa utaitamani sana kazi ya mikono yako.” (Ayubu 14:14, 15) Ayubu alikuwa na uhakika kwamba Baba yake mpendwa wa mbinguni angetamani sana kumfufua. Je, Mungu amebadilika? Biblia inajibu hivi: “Mimi ni Yehova; sikubadilika.” (Malaki 3:6) Mungu bado anatamani kuwaona wafu wakifufuliwa na kuishi tena wakiwa na afya nzuri na furaha. Ni sawa tu na jinsi ambavyo mzazi mwenye upendo angetamani kumfufua mtoto wake mpendwa. Tofauti ni kwamba, Mungu ana uwezo wa kufanya chochote apendacho.—Zaburi 135:6.

Kifo ni kibaya, hata hivyo Mungu ana suluhisho kamili

Yehova atamwezesha Mwana wake kuwaletea shangwe nyingi wale wote wanaoomboleza kwa sababu ya kufiwa na wapendwa wao. Yesu anahisije kuhusu ufufuo? Kabla ya kumfufua Lazaro, Yesu alihisi uchungu moyoni kama walivyohisi dada na marafiki wa Lazaro, naye “akatokwa na machozi.” (Yohana 11:35) Pindi nyingine, Yesu alikutana na mjane wa Naini, aliyefiwa na mwana wake pekee. Yesu “akamsikitikia, akamwambia: ‘Acha kulia.’” Kisha akamfufua mwana huyo. (Luka 7:13) Hivyo, Yesu anajua vizuri huzuni na uchungu wa kufiwa. Yesu atafurahi sana wakati atakapowaondolea huzuni wanadamu ulimwenguni pote!

Mwanamume akimkumbatia binti yake

Je, umewahi kuhuzunika? Huenda ukahisi kwamba kifo ni tatizo lisilo na suluhisho. Hata hivyo kuna suluhisho. Nalo ni ufufuo ambao Mungu atatekeleza kupitia Mwana wake. Kumbuka kwamba Mungu angependa uone hilo litakapotendeka. Angependa uwepo ili kuwapokea wapendwa wako wanapofufuliwa. Hebu wazia ukipanga mambo pamoja nao kwa ajili ya wakati ujao, milele!

Lionel, aliyenukuliwa mapema, anasema hivi: “Hatimaye, nilijifunza kuhusu ufufuo. Mwanzoni, ilikuwa vigumu kuamini, na sikumwamini aliyeniambia jambo hilo. Lakini nilichunguza jambo hilo katika Biblia na kutambua kwamba lilikuwa la kweli! Ninasubiri kwa hamu sana kumwona tena babu yangu.”

Je, ungependa kujua mengi zaidi? Mashahidi wa Yehova wangependa kukuonyesha katika Biblia kwa nini wanaamini kwamba kutakuwa na ufufuo wakati ujao.b

a Ili kuwa na uhakika kwamba Yesu alifufuliwa, soma kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? ukurasa wa 78-86, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

b Tafadhali soma sura ya 7 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki