Yaliyomo
JUMA LA JUNI 27, 2016–JULAI 3, 2016
3 Suluhisha kwa Upendo Hali ya Kutoelewana
Kwa kuwa sisi si wakamilifu, tunakabili hali zinazotuumiza kihisia. Makala hii inaonyesha jinsi tunavyoweza kutumia kanuni za Biblia ili kusuluhisha kutoelewana kati yetu.
JUMA LA JULAI 4-10, 2016
8 “Nendeni Mkafanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote”
Makala hii inazungumzia mambo yanayothibitisha kwamba Mashahidi wa Yehova ndio kikundi pekee cha watu duniani kinachotimiza unabii ambao Yesu alitoa katika Mathayo 24:14. Pia, inaeleza maana ya kuwa “wavuvi wa watu.”—Mt. 4:19.
JUMA LA JULAI 11-17, 2016
13 Ni Nini Kinachokuongoza Unapofanya Maamuzi ya Kibinafsi?
Unapofanya maamuzi ya kibinafsi, je, wewe hufanya kile ambacho unafikiri kinafaa? Au, je, wewe huwauliza wengine kile ambacho wangefanya? Makala hii inaeleza jinsi kuongozwa na maoni ya Yehova Mungu kunavyotusaidia kufanya maamuzi ya hekima.
JUMA LA JULAI 18-24, 2016
18 Je, Bado Biblia Inabadili Maisha Yako?
Je, unaona kwamba sasa ni vigumu kwako kuboresha sifa za Kikristo kuliko mabadiliko makubwa uliyofanya kabla ya kubatizwa? Makala hii inaeleza kwa nini ni vigumu kufanya hivyo, na vilevile jinsi Neno la Mungu linavyoweza kutusaidia tusitawishe sifa za kiroho.
JUMA LA JULAI 25-31, 2016
23 Faidika Kikamili na Chakula cha Kiroho Kutoka kwa Yehova
Makala hii inatuonya kuhusu mtego unaoweza kufanya tusifaidike na chakula cha kiroho. Tutachunguza jinsi ya kuepuka kunaswa na mtego huo, na jinsi tunavyoweza kufaidika na chakula chote cha kiroho tunachopokea.